Tunaishi
katika hii dunia kwa jinsi ya mwilini na rohoni
pia tunatumia akili na nguvu ili kufanikisha shughuli zetu. Kuna wakati
tunatumia nguvu sana kuliko akili, na kuna wakati pia tumia akili sana kuliko
anguvu hata wakati mwingine vyote vinatumika pamoja.
Tunapo
ongelea akili tunaongelea ufahamu na maarifa ya mambo flani, pia kuhusu mwili,
roho na nafsi; navyo vinatakiwa vifanikiwe kwa namna flani. Mtume Yohana
atatutakia heri akisema mpenzi naomba
ufanikiwe kama nafsi yako ifanikiwavyo. Mungu anatamani tufanikiwe ki mwili
,roho, nafsi,na akili.
Je
tutawezaje kufanikiwa?
YOHANA 3 : 3 Yesu akajibu akamwambia amin, amin, nakuambia, mtu asipozaliwa mara ya pili, awezi kuuona ufalme wa Mungu.
Katika
kitabu cha yohana tunakutana na hii stori ya mfarisayo aitwaye Nikodemo ambaye
alikuwa mkuu wa dini ya wayahudi na pia ukiendelea mbele Yesu anatutambulishia
kuwa huyu mtu alikuwa ni mwalimu wa Israel. Kwaiyo alikuwa anaufahamu na
maarifa kuhusu mambo flani flani. Hatukuambiwa alikuja kwa madhumuni gani
kumuona Yesu lakini tunaona kuwa Yesu alimjibu kuhusu kuzaliwa mara ya pili. Kwa
maana alijua ya moyoni mwake kabla hajauliza
Tunaweza tukasema kuzaliwa kwa mara ya
pili ni kumkiri Yesu kuwa Bwana na
Mokozi wa maisha yako na kulifata jinsi Neno lake linavyosema na kuishi jinsi
alivyotaka tuishi na kubatizwa kwa maji na Roho mtakatifu yaani kuuzika utu wa
kale na kufufuka na utu mpya.,
FAIDA
YA KUZALIWA MARA YA PILI.
1.
Kusamehewa dhambi
Ukizaliwa mara ya pili unakuwa ndani ya kristo na unakuwa kiumbe kipya na Mungu wa mbinguni anasamehe dhambi zako na kukuweka ndani ya pendo lake ambalo ndani yake kuna Baraka na neema,ukisoma 2WAKORITHO 5:17 inasema Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya kristo,amekuwa kiumbe kipya, ya kale yamepita; Tazama! Yamekuwa mapya
2.
Kuhesabiwa Haki
1YOHANA 2:29 inasema kama mkijua ya kuwa yeye ni mwenye haki, jueni ya kuwa kila atendae haki amezaliwa na yeye
Tunajua
kuwa tunahesabiwa haki kwa imani; kama
haujazaliwa mara ya pili huwezi kuhesabiwa haki kwa kuwa sheria inakufunga.
Lakini ashukuriwe Mungu baba aliye mtoa mwana wa pendo lake takatifu {YESU}
kufa pale msalabani kwa ajili ya dhambi zetu ili zambi zetu zoote ziingie kwake
ndani ya mwili wake na baada ya mateso yote na akasema IMEKWISHA. Kwaiyo ndugu
kama Yesu alimaliza yote pale msalabani sisi tuliozaliwa mara ya pili
tunahesabiwa haki kwa imani.
3.
Hutokufa
bali utaishi
tunasoma katika MATHAYO 27: 51 -53 anasema Na tazama pazia la hekalu likapasuka vpande viwili toka juu hata chini ; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka; 52 makaburi yakafunuka; ikainuka miili mingi ya watakatifuwalio lala; 53nao wakiisha kutoka makaburini mwao, baada ya kufufuka kwake, wakauingia mji mtakatifu, wakawatokea wengi.
Tunaweza kujiuliza kivipi? YESU alivyo fufuka, akufufuka peke yake alifufuka na wafu waliokufaga zamani wale walio wake yaani watakatifu. Kwaiyo tukifa katika mwili huu tunakwenda directly mbinguni tukisubili ile siku kuu ya mwana wa adamu kuja ulimwenguni kwa mara ya pili. 1YOHANA 4: 9b inasema ili tupate uzima kwa yeye
Faida
ziko nyingi sana na sana ambazo
utazipata kwa kulisoma neno lake.
Rafiki
Kama
ujampokea Yesu kuwa BWANA na mwokozi wa maisha yako nakuomba useme kwa sauti na
kwa kwa kumaanisha na kuamini moyoni mwako maneno haya.
BWANA
YESU NAKUJA MBELE ZAKO, MIMI NILIE NA DHAMBI
SIKUSTAHILI
KUISHI SIKU YA LEO, LAKINI NI NEEMA YAKO NA REHEMA,
NATUBU
ZAMBI ZANGU, NILIZOZIFANYA KWA KUNENA KWA KUTENDA NA KUWAZA
NAOMBA
UNISAMEHE MIMI NILIE NA DHAMBI, NAKIRI KUWA WEWE NI BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA
YANGU, FUTA JINA LANGU KWENYE KITABU CHA
HUKUMU, ANDIKA JINA LANGU KWENYE KITABU CHA UZIMA. ASANTE YESU KWA KUWA UMENIOKOA. AMEN
Kama umesema hayo maneno, hakika Mungu
amekusamehe kabisa na amesahau dhambi zote ulizofanya , unatakiwa uende kanisa
lililo kalibu nawe ili upate mafundisho na kukua kiroho.
MUNGU AKUBARIKI……
.