Tuesday, September 27, 2016

MAMBO YA KUFANYA ILI FIKRA ZAKO ZITUMIKE KUFANIKISHA MAISHA YAKO


amen


 SEMINA YA NENO LA MUNGU ILIYOFUNDISHWA NA MWALIMU CHRISTOPHER MWAKASEGE JIJINI DAR ES LAAM.

SOMO: MAMBO YA KUFANYA ILI FIKRA ZAKO ZITUMIKE KUFANIKISHA MAISHA YAKO

Lengo
Kuweka ndani yako maarifa ya Kibiblia yatakayokuwezesha kutumia fikra zako ili ufanikiwe ktk maisha yako

Mith 23:7(a)
Tafsiri zingine neno aonavyo nafsini mwake:-

1. afikirivyo nafsini mwake
2. awazavyo nafsini make
3. anavyotafakari nafsini mwake

Mara nyingi kwenye Biblia utakuta fikra imeandikwa fikira ni neno lilelile










MAANA YA FIKRA
Ni mkusanyiko na mtiririko wa mawazo unaotengeneza maimamo wa kiutekelezaji ndani ya mtu.

UNAJIFUNZA NINI AU UNAPATA NINI KUTOKA KWENYE TAFSIRI HIYO YA FIKRA

Ulivyo kimaisha iwe kiroho au kimwili ni matokeo ya jinsi uonavyo/ufikirivyo nafsini mwako.

2Ulivyo kimaisha inaonyesha kiwango chako cha kufikiri kilipo au kilipofikia

3Fikra ziliumbwa zikae ndani ya nafsi ili zitumike kuweka aina na kiwango cha maisha ya mtu ktk eneo linalomuhusu!
Kumbuka mtu ni roho anayo nafsi anakaa ktk mwili. Nafsi ni kiungo cha kati kati ya roho na mwili kuweza kusaidia kutafsiri roho kuishi ktk ulimwengu wa mwili bila shida na mwili kuishi ktk ulimwengu wa roho vivyo hivyo.
Ndani ya nafsi kuna fikra na akili pia
Ndani ya mwili kuna ubongo

Kwa hyo kiwango cha kufanikiwa kimewekwa kwenye nafsi=fikra

4Tofauti ya aina ya viwango Vya maisha kati ya mtu na mtu inatokana na sehemu kubwa na utofauti wao wa kufikiri


2Kor 11:3

Shetani akitaka kukumaliza aanzi kwenye roho bali uenda moja kwa moja kwenye nafsi=uvuruga fikra zako kwanza

Kwenye Bustani ya Eden alivuruga fikra zao kwanza vivyo hivyo kwenye swala la mtu kuokoka kule kusitasita na kuamua vinginevyo ni fikra uvurugwa kwanza.


HATUA AMBAZO UNAHITAJI KUZIFUATA KAMA UNATAKA KUTUMIA FIKRA ZIKUSOGEZE KIMAISHA

1Tasmini maisha yako I'll ujue kiwango cha kufikiri kwako kilivyo

Haijalishi mahali ulipo au maisha uliyonayo mazuri ama la
Itakusaidia ujue unaanzia wapi ktk kushughulika na kufikiri kwako
Kama unataka kwenda na BWANA kwenye jambo lolote jifunze kuanza na kuwa unajitathimini kila wakati!
Wengi ujiuliza natumia vigezo gani kujitathimini?
Kiblia kigezo cha maisha ni Agano
Ndani ya Agano YESU KRISTO aliweka viwango Vya maisha ambavyo vitatusaidia ktk tathimini


MIFANO YA KUJIFUNZA HAPA

2Falm 4:1-7
Maisha ya mama mjane tuyatafakari ili tuweze kujua kiwango cha kufikiri kwake

TUNAONA MAMBO YAFUATAYO

1. Fikra zake za kimaisha zilikwamia mahali zilipokwamia fikra za mume wake.
Maana yake hakuwa na mawazo ya kimaisha zaidi ya yale ya mume wake mpaka pale mime wake alipofariki.
KIVIPI
-Sababu fikra hazipo hakuwa na hakujua kitu cha kufanya ndo maana alimwendea Elisha.
Ile kwamba umeolewa haifanyi kwamba akili yako isifanye kazi au ya mime wako ndiyo sahihi na superior tu.

2. Hali ya maisha na kiwango cha maisha cha mama mjane na watoto wake kilitokana na ulipofika mtiririko na mkusanyiko wa fikra za mume wake.
Ukitaka kujua yule baba alifikirije angalia maisha ya familia take
Kuishi kwako ni matokeo ya kufikiri kwa baba yao.
Umaweza ukawa na maisha mazuri kumbe ni fikra ya kampuni unayofanyia kazi

3. Fikra za mume wake zilitengeneza viwango Vya maisha yake na familia kutoka kwenye maeneo haya yafuatayo:-
(a) Kulitegemea Utumishi wake aliokuwanao kwa Elisha
(b) Kumcha BWANA ilikuwa ni kigezo cha maisha yao
(c) Alikuwa anaishi kwa mkopo na ambao alikufa hajaumaliza

Kumbuka Utumishi hautengenezi maisha yako Bali FIKRA
Biblia haikatazi mkopo bali deni
Usifurahia uchaji tu ulionao kama uchaji huo hauwezi kuchaji fikra zako huwezi kufanikiwa kimaisha japo mbinguni utaenda.

4. Mume wa mjane alimjengea mkewe kufikiri ya kuwa maisha yao yalitokana na ushauri na mwongozo wa Elisha na kumbe siyo

5. Mama mjane hakujua cha kufanya juu ya fikra za mume wake ya kuwaweka watoto rehani
Aliwaweka watoto rehani maana yake alikuwa anawajengea watoto wake fikra za utumwa

6. Fikra zake na mume wake hazikuwa na uwezo wa kutumia walichokuwanacho ili kuwatengenezea maisha mazuri.

HOME WORK
Jiulize maswali haya

1Jiulize nini chanzo cha kipato chenye kufanya uwe jinsi ulivyo?

2Je chanzo hicho kikiondoka/kutoweka je maisha yako yatakuwaje?


3Fikra zako zinahusika kwa kiwango gani ktk kupatikana kwa kipato hicho?

No comments:

Post a Comment

Makala nyingine

IMPORTANCE OF OUR TESTIMONIES IN THE CHURCH

Mathayo 8:1-4 Naye aliposhuka mlimani, makutano mengi walimfuata.  Na tazama, akaja mtu mwenye ukoma akamsujudia, akisema, Bwana, u...