MHUBIRI
3:1-8 ukisoma huo mstari utajifunza kuwa Kuna wakati kwa kila kitu
kilichopo duniani..,Mungu aliviumba vitu katika mifumo tofauti ambazo zinaenda
kwa muda na wakati.
Na kuna nyakati na misimu kwa
kila shughuli zinzo fanyika duniani
Mfano kipindi cha masika na
kiangazi
Binadamu naye ameubwa katika
kupita katika vipindi tofauti , ndo mana biblia inasema kila jambo na wakati
wake. Kuna wakati mwanadamu anapita katika majonzi ,lakini hayatokuwa ni maisha
yake yote, na kunawakati mwanadamu anapita kwenye furaha lakini haitakuwa
maisha yake yote.
Kuna majira lazima mwanadamu
apite ili yamfundishe na kumfanya awe jasiri akikutana na changamoto kama hile iliyopita
MWANZO 1:14
.Mungu akasema, “Iwepo mianga kwenye
nafasi ya anga ili itenganishe mchana na usiku, nayo
iwe alama ya kutambulisha majira mbali mbali, siku na
miaka,
Nataka tutazame alipo sema
ALAMA …hapa tunaona kuwa Mungu aliweka
sign kwa kila majira yanayotaka kutokea , ni sawasawa na kwa mwanadamu kila changamoto inayotaka kutokea
maishani mwako lazima kuwe na alama, iwe umeokoka au ujaokoka, Kwa sisi tulio okoka Roho wa
Bwana ndie hutupa ALAMA za majira na nyakati.
MUWEKE YESU ASHIKILIE MUDA
WAKO
kwamba mpango wa Mungu kwa
mwanadamu ni Mzuri, mwanadamu alijichanganya na kutofautiana na Mungu pale
alipotenda dhambi, na kuna majira yaliwekwa kuwa ATAFANIKIWA KWA JASHO LAKE MWENYEWE ,
Tunajua kuwa hii hali ilikuwa
ni ngumu sana , lakini Mungu wa Israeli akamtuma mwanawe wa pekee yesu kristo aje duniani ktupa
ukombozi na ile neema itoka nayo na ukombozi,
Kwa mtu ambaye amemkiri Yesu
kuwa ni Bwana na mokozi wa Maisha yake, Yesu anakuwa ni kiongozi au dereva wa
majira na nyakati zilizo wekwa maishani mwako. Na kila changamoto itakayo tokea
Roho mtakatifu atakujulisha ili ufanye maombi .
Tena yesu awezi kukuacha
katika changamoto unazopitia kwa kuwa umemueka yeye awe kiongozi wako wa kila
kitu.
ISAYA 60:19-20
19Jua halitakuwa tena nuru yako mchana,
wala mwangaza wa mwezi
hautakuangazia,
kwa maana BWANA atakuwa nuru
yako ya milele,
naye Mungu wako
atakuwa utukufu
wako.
20Jua lako halitazama tena,
nao mwezi wako hautafifia tena,
BWANA atakuwa nuru yako milele,
nazo siku zako za huzuni zitakoma.
Hapa tunajifunza vitu vingi sana , kimoja wapo ni Yesu atakuwa utukufu wako, kivipi ?
pale utakapo muweka awe kiongozi wako kwenye kila
kitu, hata kwenye masomo
Nimeona wanafunzi wengi
wakiwa bize na time kwenye kusoma but wanamsahau yesu ambaye anauwezo wa
kubadilsha mawazo na upeo wa akili zao kwa sekunde chache.
Pia tunaona kuwa watu wengi
hutazama jua na mwezi na hata nyota kujua nyakati na majira lakini pale utakapo
mweka Yesu mbele, utukufu utaonekana katika majira yote utakayo ishi.
Pia unakuta mwanafunzi
anajali muda wa kusoma kuliko kufanya maombi,kuliko kusoma biblia angalau
kwa nusu saa. Ukimweka Yesu awe kiongozi
katika muda wako, Hakika atakuwa utukufu wako na hata katika siku
zako za shida Yesu ataziondoa kwa kuwa umemuweka yeye awe kiongozi wa muda wako
YOHANA 1:1-4
Hapo mwanzo, alikuwako Neno.
Huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. 2Tangu
mwanzo huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu.
3Vitu vyote viliumbwa kwa Yeye, wala pasipo Yeye hakuna cho chote
kilichoumbwa ambacho kimeumbwa. 4Ndani Yake ndimo ulimokuwa uzima na huo
uzima ulikuwa nuru ya watu.
Katika mistali hii tunaona
kuwa Yesu kristo alikuwako tangu mwanzo wa kuumba dunia, tena ndani yake kunako
uzima na milele na huo uzima ndio nuru ya watu… kwa hiyo kama uzima ni nuru ya
watu basi katika uzima anaotoa yesu ndipo tutafanikiwa kuukomboa wakati na
majira… kitakacho tusaidia ni kufanya maombi kwa bidii.
No comments:
Post a Comment