YEREMIAH 1:5
Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.
Uongozi
na usimamizi ni kitu ambacho wote tunatakiwa kujua na kuelewa, kwako kinaweza
kuwa kipya au ulishawahi kwenda
ulifanikiwa kujifunza kwenye taasisi au chuoni.
Kila mtu amezaliwa kuwa kiongozi na tunatakiwa
kutumia skills hii katika kazi zetu na tuwajibike iwe kanisani au katika jamii
au hata nyumbani
Kama
unataka kuwa msimamizi au kiongozi mzuri ni vema uanze kufanya kwa vitendo
katika shughuli zako za kila siku iwe nyumbani au katika shughuli za kawaida.
· Kiongozi
huwa anaonesha uelekeo na ku inspire timu kufanya kazi ili wafikie lengo
husika, kumbuka kiongozi lazima kila siku awe anajifunza
· Hakikisha
kila mtu unaemuongoza ajue mawazo yako
na kuamini kuwa hicho kitu unachowaongoza kitafanikiwa
· Pia
tengeneza wingu la furaha katika mazingira mnayofanyia kazi ili kila
unaemuongoza ajisikie kuwa ana thamani.changamoto ikitokea jitahidi kuwa fear kwa kila mfanyakazi.
· Changamoto
ikitokea wewe ndo uwajibike , usijalibu kumlaumu mtu unaye moungoza zaidi unatakiwa kumkumbusha ni kitu gani afanye na ikibidi muonye kwa upole.
· Pia
jitahidi kujenga team work yenye nguvu katika watu wako na ushirikiano mzuri.ili kama kuna mapungufu ,watu unaowaongoza waweze kukusaidia kimawazo na kuafanya kazi kwa moyo wa kupenda.
BIBLIA INASEMAJE?
Kiongozi lazima uwe una hofu ya
Mungu ili kuongoza watu katika maadili mema, hakikisha unaongoza sawasawa na
mpango wa Mungu ili uweze kupata kibali mbele za wanadamu na Mungu mwenyewe
Kumbuka katika uongozi, kiongozi
wako mkuu ni Mungu mwenyewe, usiogope
wanadamu maana si kila mwanadamu
anapenda umuongoze isaya 41:10
Kinachoitajika katika uongozi wako
ni kujinyenyekesha kwa Bwana,unatakiwa ujue kila siku kuwa Mungu ndiye
amekuweka mahali hapo ili atukuzwe
kupitiwa wewe, kwa kuwa amekuchagua kama mtumishi wake jua atazidi kukuinua juu
kila itwapo leo.
Sawa tunaweza kuwa watumishi wa
Mungu katika uongozi lakini tunatakiwa tuwe na bidii katika kazi zetu
Tufanye kazi tukijua kwamba sisi
tuwabalozi wa YESU . Mithali 22:29
Kumbuka
kiongozi ni mfano kwa wengine . mkabidhi Bwana njia zako pia umtumaini naye
atakuafanya uwe kiongozi BORA.

No comments:
Post a Comment