ZABURI 29:11 unasema...
Bwana atawapa watu wake nguvu, Bwana atawabariki watu wake kwa amani.
Binadamu kuna wakati tunafika tunachoka kimwili na kiakili kwasababu kuna force
ambayo tunatumia kwenye shughuli flani kwaiyo inafika wakati tunachoka.
MFANO WA
KUCHOKA KWA JINSI YA KIROHO
Kwa jinsi ya rohoni kuna mstari kwenye biblia
unaniambia kuwa tunafanywa upya siku
hadi siku (2 corinthians 4:16).. hii inatukumbusha kuwa kuna wakati roho inachoka kufanya kusudi la Mungu.. na ndomaana
tunatakiwa tujifunze mambo mengi ya rohoni ili tuwe na uzoefu…tujaze mioyo yetu
neno la Mungu. Ambalo linatusaidia kujua
vitu vya rohoni… na linatusaidia kutia nguvu roho zetu ili tusichoke kuipigania
imani. Mungu akitaka kupitisha vitu anapitishia rohoni afu vina be transformed
kwenye ulimwengu wa kawaida.
MFANO WA KUCHOKA KWA JINSI YA MWILINI
Kwa jinsi ya mwilini kuna mstari kwenye biblia
unasema kusoma sana kunauchosha mwili (Ecclesiastes 12:12) pia kuna sehemu tunaona Yesu alichoka akakaa
kalibu na kisima (John 4:6) hii inaonesha kuwa kuna wakati kwa jinsi ya mwili
kama wanadamu tunachoka.. atuwezi pekee yetu tunahitaji msaada wa Mungu. Kuna
wakati unatamani kusoma vitabu lakini kila unapogusa kitabu unahisi umechoka na
unatamani ulale, sikia Mungu anakuwazia mema … Mungu anataka aanze na
kukutengeneza rohoni kwanza afu aje mwilini … ukikaa vizuri rohoni utakuwa na uwezo wa kuu control mwili wako .
Kuna wakati flani unafika mtu anakosa nguvu ya
kuomba anatamani apate nafasi ya kuomba lakini anashindwa
Kuna wakati mtu anafika anatamani asome Neno la
Mungu lakini anajikuta anashindwa
Kuna wakati mtu anafika anatamani afikie malengo ya
mafanikio katika uchumi lakini anashindwa
Na kuna wakati mwanafunzi anatamani apate nguvu ya
kusoma ili aweze kufaulu zaidi lakini anajikuta anashindwa
Rafiki hiyo hali ipo kwa kila mwanadamu hata
wanafunzi wake Yesu walishindwa kuomba na Yesu angalau lisaa limoja..sio kwamba
hawakupenda laikini walikuwa hawana
nguvu ndani yao
Jibu ni kukaa kalibu na Mungu na kumuomba akutie
nguvu ili uweze kufika hatua flani.
Tatizo sio wewe tatizo ni shetani ambaye humfanya
mtu achoke ili huyo mtu asiweze kusonga mbele na kushindania imani.
Naupenda huu mstali
nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu
(Philippians 4:13) kumbe yupo awezaye kututia nguvu
katika kila changamoto tunayo pitia ,ambaye ni YESU KRISTO WA NAZARETI kwa
maana atujua ni ya mioyo yetu. Anajua kuwa tunataka tuvuke daraja flani
ilitufanikiwe lakini anasubiri uje usemezane naye uwe kalibu yake . tena
anasema kuwa Yeye alituchagua sisi tuwe wake na tena ametununua kwa damu ya
thamani kwanini asitutie nguvu kwasababu
tumezifuata njia zetu wenyewe tumemsahau yeye .
Napenda huu mstali Huwapa nguvu wazimiao
humuongeza nguvu yeye asiye na uwezo (Isaiah
40:29) kwaiyo yeye Bwana atujua tulivyo tukimkalibia atatusaidia.
Naweza kusema kuwa Yesu ni Bwana wa viumbe vyote na
tena ni mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote
kwaiyo kama yeye ni bwana wa viumbe vyote.. nadiriki kusema nguvu za
aina yoyote zinamjua udhaifu wowote unamfahamu kwa kuwa alikuwepo kabla ya
misingi ya dunia kuwekwa. yeye ni Bwana
wa milele tena hazimii wala achoki akili
zake azichuruziki..
Wewe usiekuwa na uwezo ujue na ukili kuwa yeye ni Bwana wa
vyote katika eneo ambalo unakosa nguvu
muweke yeye naye atafanya jambo katika maisha yako.
Napenda mstari huu kwa ulivyotafsirika kingereza
My soul is weary with sorrow, strengthen me according to your word
Kuna wakati nafsi zetu zinakuwa hazina hamu wala
uzito wa kumtafuta Bwana, lakini tumeruhusiwa kumwambia Bwana vile tunavyojiona
kwamba KUPITIA NENO LAKO NAOMBA NGUVU.
Ujue Mungu
wetu ni Mungu mwema hata kama umetenda
dhambi kiasi gani, au dhambi zako zijakuwa nyekundu kama damu yeye ni mwaminifu
anasamehe na kusahau kabisa na kukutia nguvu ya kuishinda dhambi.
Mwisho naweza kusema kwamba majira haya na nyakati hizi ni za kuishi na
Yesu kwa maana Neema ingaliipo katikati yetu katika
Nehemiah
8:10 bible says that go and enjoy choice food and sweet drinks, and send some
to those who have nothing prepared. This day is Holy to our Lord. Do not
grieve, for the joy of the Lord is your strength.
kumbe furaha
ya Bwana ni nguvu kwetu Basi ilituwe na nguvu ni kufata sheria zake ili
tumfanye atufurahie .. kwa maana akifurahi. Bwana anataka tutende yaliyo mema
kamwe awezi kukuacha uangaike atakuapa nguvu za kukupa utajiri kwa maana haijawahi
kutokea mwenye haki akaachwa na wala watoto wake kulanda barabarani Mungu
anajua tunapopitia na tena anatuwazia mema anatamani tusogee kwake tutengeneze
urafiki nay eye atatutia nguvu kwenye kila kitu. AMEN

No comments:
Post a Comment