Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii.
Yak 15-16
Biblia inatufundisha vitu 3
1. Toba
2. Maombi
3.bidii
Toba
Tunafundishwa kuwa tukumbuke kuomba toba kwa ajili ya yetu na wenzetu,
Watu wengi wakienda mbele za Mungu hawakumbuki kuomba toba kwa ajili ya wengine..... , na hii hupelekea maombi yao kutojaa majibu yanayostahili katika kuomba kwao.
Tunaomba toba si kwamba tumetoka kufanya dhambi ,hapana bali unapoenda mbele za Mungu lazima ujitakase kwa maana yeye ametukuka, pia sisi sio wakamilifu kwaiyo tunaitaji damu ya Yesu ili tuweze kufika katika ukamilifu wa Mungu.
2. Maombi
Watu wengi tunapoenda kuomba huwa tunaenda kwa ajili ya maendeleo yetu na sio maendeleo ya wenzetu .
Tunaona kuwa Yesu alituombea sana kuliko kujiombea yeye, hapa anatufundisha kuwa mpende jirani yako kama nafsi yako, na hii ndio huduma ambayo Mungu anataka , maana alisema anatafuta mtu katika nchi ili alijenge boma, yaani sehemu iliyobomoka , kubomoka wapi sio kwake huyo mtu bali taifa,kanisa ,familia ,jamii ....
3. Bidii
Lakini tunaona kuwa biblia inatufundisha kuwa kuomba kwa mwenye haki kwafaa kuomba kwa bidii, kwaiyo tunatakiwa tuwe watu wa kuomba sana na kwa ufasaha,
To be continue......
No comments:
Post a Comment