Isaya 41:21
Haya, leteni maneno yenu, asema Bwana; toeni hoja zenu zenye nguvu, asema mfalme wa Yakobo.
Mungu
anatupa nafasi sisi watoto wake tuweze kuongea kile kitu ambacho tunataka
tufanye, tufanyiwe, kitokee au kisitokee.
Hoja zenye nguvu
Mungu
anatupa ruhusa ya kujadiliana naye mambo yetu ambayo tunataka kumshilikisha.
Mungu
anataka tutumie akili na moyo pale tunapo taka kusema naye,
Tunapoenda mbele za Mungu tutumie moyo ili tuweze kuweka Imani zetu kwa yeye ili tupate itaji letu.
Imani
juu ya unacho kiomba basi utapokea.
Ebrania 10 : 38
Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita, roho yangu haina furaha naye.
Imani inakaa mioyoni [ warumi 10 : 10 Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu ]
Isaya
1:18a
Haya, njoni, tusemezane, asema Bwana. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu.
Kwenye biblia ya
kingereza kasema come now let us settle the matter
Settle
: to reach a decision or an agreement about something, or to end a disagreement:
Hapa
bado Mungu anatusogeza karibu, kwa njia
ya kusolve tatizo , yaani kuyajenga, kuondoa tofauti zetu.
Mungu
wetu alituumba akatupa uhuru wa kufanya jambo,
Tuko tofauti na viumbe vingine, Ametupa nafasi sisi wanadamu wa kujielezea mbele zake na hii ndio maana ya upendo (uhuru)
Mathayo
7 :7
Ombeni,
nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa;
8 kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye
huona; naye abishaye atafunguliwa.
9 Au kuna mtu yupi kwenu, ambaye, mwanawe akimwomba
mkate, atampa jiwe?
10 Au akiomba samaki, atampa nyoka?
Bado
mungu anaonyesha ukaribu na wanadamu yakuwa chochote tutapata ila tumuombe yeye.
Kuna
vitu vitatu katika mstali huu
1. Omba
( ask)
to put a question to someone, or to request an answer from someone
2. Bisha ( knock)
to repeatedly hit something, producing a noise:
3. Tafuta
( seek )
to try to find or get something, especially something that is not a physical object:
Tunao
uwezo wa kumshawishi Mungu tukiwa na Hoja zenye nguvu.
Mathayo 11:12
Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka.
Kjv bible
Suffereth means with unwilling permission
Violent means using force to hurt or attack
Biblia
inasema ufalme wa mbinguni unapatikana kwa nguvu nao wenye nguvu wauteka
Anaposema
ufalme wa mbinguni anamaanisha;-
1. Vitu vizuri vya mbinguni
2. Mamlaka
ya kutawala ya mbinguni
3. Uhuru
ambao uko mbinguni
4. Amani
iliyokuwa mbinguni
Kuupata
kwa nguvu anamaanisha kuufanyika kazi mpaka upate,
Kuuteka
- Anaposema
kuuteka Anamaana hatupewi, ila tunachukua bila lidhaa, yaani hatukustahili
kuwanacho ila tunakuwa nacho.
- Hukustahili kupata kitu flani ila unakipata.
“Nakuombea ifike level
ambayo kuna kazi ulitakiwa kuikosa, kwakuwa unazo nguvu za rohoro uipate kwa jina la Yesu ”.
Mifano
ya watu ambao walikuwa na hoja na nguvu ambazo zilibadili mambo yao.
Ibrahimu (Mwanzo 18:19-30
19 Kwa maana nimemjua ya kwamba atawaamuru wanawe, na
nyumba yake baada yake waishike njia ya Bwana, wafanye haki na hukumu, ili
kwamba Bwana naye akamtimizie Ibrahimu ahadi zake.
20 Bwana akasema, Kwa kuwa kilio cha Sodoma na Gomora
kimezidi, na dhambi zao zimeongezeka sana,
21 basi, nitashuka sasa nione kama wanayotenda ni kiasi
cha kilio kilichonijia; na kama sivyo, nitajua.
22 Basi wale watu wakatoka huko wakaelekea Sodoma; lakini
Ibrahimu alikuwa akali akisimama mbele za Bwana.
23 Ibrahimu akakaribia, akasema, Je! Utaharibu mwenye
haki pamoja na mwovu?
24 Huenda wakawapo wenye haki hamsini katika mji,
utaharibu, wala hutauacha mji kwa ajili ya hao hamsini wenye haki waliomo?
25 Hasha usifanye hivyo, ukamwue mwenye haki pamoja na
mwovu, mwenye haki awe kama mwovu. Hasha; Mhukumu ulimwengu wote asitende haki?
26 Bwana akasema, Nikiona katika Sodoma wenye haki
hamsini mjini, nitapaacha mahali pote kwa ajili yao.
27 Ibrahimu akajibu, akasema, Basi, nimeshika kusema na
Bwana, nami ni mavumbi na majivu tu.
28 Huenda wakapunguka watano katika wale hamsini wenye
haki, je! Utaharibu mji wote kwa kupungua watano? Akasema, Sitauharibu, nikiona
humo arobaini na watano.
29 Akazidi tena kusema naye, akinena, Huenda wakaonekana
humo arobaini? Akasema, Sitafanya kwa ajili ya hao arobaini.
30 Akasema, Bwana asiwe na hasira, nami nitasema, Huenda
wakaonekana huko thelathini? Akasema, Sitafanya, nikiona humo thelathini.
Musa
(Kutoka 32:9-14
9 Tena Bwana akamwambia Musa, Mimi nimewaona watu
hawa, na tazama, ni watu wenye shingo ngumu
10 basi sasa niache, ili hasira zangu ziwake juu yao,
niwaangamize, nami nitakufanya wewe uwe taifa kuu.
11 Musa akamsihi sana Bwana, Mungu wake, na kusema,
Bwana, kwa nini hasira zako kuwaka juu ya watu wako uliowaleta kutoka nchi ya
Misri kwa uweza mkuu, na kwa mkono wenye nguvu?
12 Kwa nini Wamisri kunena, wakisema, Amewatoa kwa
kuwatenda uovu, ili apate kuwaua milimani, na kuwaondoa watoke juu ya uso wa
nchi? Geuka katika hasira yako kali, ughairi uovu huu ulio nao juu ya watu
wako.
13 Mkumbuke Ibrahimu, na Isaka, na Israeli, watumishi
wako, ambao uliwaapia kwa nafsi yako, na kuwaambia, Nitazidisha kizazi chenu
mfano wa nyota za mbinguni; tena nchi hii yote niliyoinena nitakipa kizazi
chenu nao watairithi milele.
14 Na Bwana akaughairi ule uovu aliosema ya kwamba
atawatenda watu wake.
Mfalme
Hezekia (Isaya 38:2-6)
2 Basi Hezekia akajigeuza, akaelekeza uso wake
ukutani, akamwomba Bwana,
3 akasema, Ee Bwana, kumbuka haya, nakusihi, kwamba
nimekwenda mbele zako katika kweli na kwa moyo mkamilifu, na kutenda yaliyo
mema machoni pako. Hezekia akalia sana sana.
4 Ikawa, neno la Bwana likamjia Isaya, kusema,
5 Enenda ukamwambie Hezekia, Bwana, Mungu wa Daudi, baba
yako, asema hivi, Mimi nimeyasikia maombi yako, nimeyaona machozi yako; tazama,
nitaziongeza siku zako, kiasi cha miaka kumi na mitano.
6 Nami nitakuokoa wewe, na mji huu, na mkono wa mfalme
wa Ashuru, nami nitaulinda mji huu.
Hannah
(1 Samweli 1:14-20)
14 Ndipo Eli akamwambia, Je! Utakuwa mlevi hata lini?
Achilia mbali divai yako.
15 Hana akajibu, akasema, Hasha! Bwana wangu, mimi ni
mwanamke mwenye roho ya huzuni, mimi sikunywa divai wala kileo, ila nimeimimina
roho yangu mbele za Bwana.
16 Usimdhanie mjakazi wako kuwa ni mwanamke asiyefaa
kitu; kwa kuwa katika wingi wa kuugua kwangu na kusikitika kwangu ndivyo
nilivyonena hata sasa.
17 Ndipo Eli akajibu, akasema, Enenda kwa amani; na Mungu
wa Israeli akujalie haja yako uliyomwomba.
18 Naye akasema, Mjakazi wako na aone kibali machoni
pako. Basi huyo mwanamke akaenda zake, naye akala chakula, wala uso wake
haukukunjamana tena.
19 Wakaondoka asubuhi na mapema, wakasali mbele za Bwana,
kisha wakarejea na kufika nyumbani kwao huko Rama; Elkana akamjua mkewe Hana;
naye Bwana akamkumbuka.
20 Ikawa, wakati ulipowadia, Hana akachukua mimba na
kuzaa mtoto mwanamume; akamwita jina lake Samweli, akisema, Kwa kuwa nimemwomba
kwa Bwana.
Yabesi (1 Nyakati 4:9:10)
9 Naye Yabesi alikuwa mwenye heshima kuliko nduguze;
na mamaye akamwita jina lake Yabesi, akisema, Ni kwa sababu nalimzaa kwa
huzuni.
10 Huyo Yabesi akamlingana Mungu wa Israeli, akisema, Lau
kwamba ungenibarikia kweli kweli, na kunizidishia hozi yangu, na mkono wako
ungekuwa pamoja nami, nawe ungenilinda na uovu, ili usiwe kwa huzuni yangu!
Naye Mungu akamjalia hayo aliyoyaomba.
Nakuombea yakuwa Mungu azidi kukufungulia Neema ya kuisikia sauti yake. AMEN
No comments:
Post a Comment