2Falm 4:1-7
✅kipengelea cha muhimu au nataka uone hapa ni pale
Biblia inaposema....... enenda ukayauze mafuta haya.........
✅Ningekuwepo kipindi hiki ROHO MTAKATIFU anamvuvia
upako mwandishi wa kitabu hiki ningemwambia aongeze kidogo hii habari ya mama
mjane kujua jinsi alivyouza mafuta haya maana Biblia haikuendelea kusema
✅Maana hakuwa mfanyabiashara, alikuwa mgeni sokoni, ni
mara yake ya kwanza kuuza
✅Je somo la kuuza alipata wapi? Je aliuza? Kwa shs
ngapi?
✅Maana waweza kuwa na vitu na usiuze pia maana si kitu
chepesi atii, wafanyabiashara wanaelewa. Jiulize Mama mjane hakuwa na hata na
lebo kwenye mafuta yake, packing ilikuwa na kumbuka vyombo vilikuwa vya kuazima
maana yake mafuta yako kwenye vyombo tofauti tofauti, alifungajefungaje?
JAMBO LA MSINGI
✅Ni kuwa Elisha alitumika kumtengenezea kuandaa FIKRA
zake zaidi kwa habari ya soko.
FUNZO LA SITA
Jifunze na jizoeze kulitafuta
na kuliona na kuliingia soko kiroho kwanza kwa njia ya FIKRA zako kabla
ujaliona soko hilo
iwe kimwili ama kiuchumi
➡Utekelezaji
wa mstari wa 7 unategemea sana
utekelezaji wa ile mistari.kuanzia wa 3-6
➡mistari
ya 3-6 Alitekeleza kwa kiwango gani maagizo aliyopewa
➡Maana
3-6 maagizo haya yalikuwa ya kujenga FIKRA zake ziweze kuona thamani ya chupa
ya mafuta kwa jicho la FIKRA zake.
➡Ndani
ya FIKRA zake lazima uhitajiwa (soko) wa chupa ya mafuta
➡MUNGU
alimtengenezea ya kuwa kama ulichonacho hakina
thamani kwenye FIKRA zako hakiwezi kuwa na thamani kwenye soko
SABABU HIYO
✅FIKRA lazima zione thamani ya kitu(uhitajiwa wake)
ndiyo kitakuwa na thamani sokoni
✅Wengi wamekufa na kuviacha vitu vingi sana sababu ya kushindwa
kitambua uthamani wake hata hivi leo kupotea bila faida
✅Soko linaonekana kwanza kwenye FIKRA kabla ya nje
Wakati mama mjane anapewa
maelekezo aliambiwa
I). Nenda, halafu koma(,)
Maana yake fikra zake ziwe na
utayari wa kutafuta soko. Yalikuwa maamuzi ya ndani
II). Nenda ukatake vyombo kwa
jirani zako wote
✅Alikuwa anaambiwa panua wigo wa vyombo vitupu
✅MUNGU alitaka aone uhusiano wa chupa ya mafuta na
FIKRA zake pamoja na soko la mafuta
✅Kati ya chupa ya mafuta na soko la mafuta katikati
yake kuna FIKRA
✅FIKRA zikigoma soko la mafuta limegoma
✅Kwa hiyo uhusiano kati ya chupa ya mafuta, FIKRA na
soko ni wa KIROHO KWANZA .
✅Kwa lugha nyepesi Soko ni mkutaniko wa wauzaji na
wanunuzi
✅Mtu anayeuza anategemea soko kuuza, soko kumkutanisha
na mnunuzi, soko kumpa bei, soko kumwandalia auze lini kwa kiasi gani
✅Anayenunua naye anategemea soko limkutanishe na bidhaa
anayoitahi, soko limpe bei, limkutanishe na muuzaji, limwekee utaratibu wa
kununua
SOKO LINAANDALIWA NA NANI
➡Wauzaji/muuzaji
➡Mununuzi
➡Wote
kwa pamoja
➡Yule
ambaye upata faida kwa Mnunuzi na Muuzaji kukutana (Serikali)
✳Soko
linatakiwa kutawalina na nani? Na linatawaliwa na nani?
✅Soko uandaliwa kwenye FIKRA (msukumo wa kuhusisha
ulichonacho na soko)
✅Soko ni la KIROHO KWANZA
Isaya 24:1-2
✅Adhabu ya kiroho ilienda kugusa maeneo tofautitofauti
imegusa mpaka soko
-Muuzaji na Mnunuzi
wanafanana
-Mkopaji na Mkopeshaji
wanafanana
EZEKIEL 7:12
➡Muuzaji
na Mnunuzi kuna adhabu mjini
NEHEMIA 13:15-22
➡Viongozi
kutumia misingi yao
ya imani kubana aina fulani ya soko
➡Kiongozi
alifunga milango kuzuia biashara sababu ya misimamo yake ya kiimani
✅Kwa hiyo nguvu ya hilo soko halipo ktk vitu vinavyouzwa bali
ktk ulimwengu wa roho
✅Imani kuanza kuingia kidogo kidogo kwenye uchumi kuwa
na uhakika utegemea ni imani ipi na ina ingiza nini ndo maana soko uanzia
rohoni kwanza.
UfUNUO 13:1-7
➡Roho
ya mpinga kristo ukimbilia kushambulia kwenye eneo la soko
➡Ndo
maana watu.wenye haki/walokole wengi wanapambana hapa shetani anajaribu
kuwazuia kwenye eneo hili ili wasifanikiwe na wengine hawajui kwanini kila
biashara kwako inagoma au yeye auzi na wale wenzake wa mataifa wanauza kweli.
Shida ni kutokujua na kutofundishwa kuona soko rohoni kwanza.
SWALI
Wangapi hawana Akaunti Benki?
Ila wengi hawajui kwanini hawataki kugungua akaunti benki. Sasa sikwambii huna
pesa au napigia debe Benki noo
Mfano Mfanyakazi unapokea
mshahara ukatoa sadaka zako na kilichobaki kikarudi benki uwe na uhakika
kimerudi na ROHO wa MUNGU kwenye mzunguko wa fedha yako
➡Pesa
haina dini bali ina Roho.
Uf 18:1-3,9-13
➡Hakuna
mtu anayenunua bidhaa yao
tena si kwamba soko halipo
➡Si
kila mfanyabiashara utafuta msaada sehemu nzuri
➡Kuna
anaye amua kipi kinunuliwe na kipi kisinunuliwe usipoweza kujua hapo na
kutengua hapo utateseka
NANI ANATAWALA SOKO LA AJIRA?
➡Ulimwengu
wa roho utawala soko hili
Jifunze kwa kina Daniel
walikuwa bora mara 10 ya wale waliomzunguka mfalme! Maana mfalme hakuwa na
kauli ya mwisho na sababu kina Daniel walikuwa bora zaidi kilimbana mfalme
kuwaondoa wale wachaw na nafasi hizo kupewa kina Daniel.
Uf 5:9-10
....ukamnunulia MUNGU.....
✅DAMU YA YESU ina ruksa kuingia sokoni sababu kuna kitu
kilichokuwa kinauzwa kimewekwa bei ya juu ili kisinunuliwe
✅YESU alijua thamani ya DAMU yake na alitununua kwa
cash.
✅Kwa kutumia DAMU ya YESU waweza ingia kama mfalme sokoni
✅Usijizuie omba kila ufikapo dukani kwako anza kwa
maombi
✅mahali ambapo soko halina haki kuna dhuruma na mambo
si ya KIFALME achilia DAMU ya YESU isemeshe ardhi ya mahali hapo
✳Usiende
kwenye soko bila DAMU ya YESU
✳Hakikisha
FIKRA zako zimepata kibali cha NENO la MUNGU na ROHO MTAKATIFU
✳Ombea
kibali juu ya Biashara yako
✳Hakika ROHO MTAKATIFU anajua anayehitaji bidhaa
unazouza
Math 6:33
➡Hakikisha mfumo wa UFALME wa MUNGU umekaa juu ya soko
➡Mfumo.unatengenezwa, tafuta haki mfumo wa Kiblia wa
Biashara (soko) uliopotea
➡Maana bila mfumo hakuna uwajibikaji. Mfumo.wahitajika
kila mahali iwe kanisani mpaka kwenye familia..
HOME WORK
✳Unaona soko kwenye FIKRA zako kwa kiwango kipi?
(Fursa zako za kuuza na
kununua na kuuza tena)
✳Cheki mahali unapofanyia Biashara kama
kuna umiliki wa KIROHO/KIFALME
No comments:
Post a Comment