Tuesday, September 27, 2016

SOMO LA FIKRA PART 4.


HATUA AMBAZO UNAHITAJI KUZIFUATA KAMA UNATAKA KUTUMIA FIKRA ZIKUSOGEZE KIMAISHA

Tumeshaangalia hatua 2 tuko tumeanza seminar. Leo tuendelee na ya 3

3Panga FIKRA zako kwa upya ili zisikupitishe tena mahali pabaya ulipokwisha pitia.

FIKRA zinapangika
Mfano kwa mama mjane baada ya kusaidiwa na Elisha akitaka hali ile ya mwanzo isijirudie tena lazima abadiri kufikiri kwake la sivyo ile hali atarudi tu

2Falm 5:7
Mama mjane alipanga FIKRA zake kwa upya..lazima ujifunze kupanga FIKRA zako kwa upya
Tuonaona mstari wa 7

...Nenda kauze mafuta...
Si FIKRA tu kutumika bali MUNGU alitaka Mama mjane ajuaje na akubali ndani yake kuwa MUNGU ndiye amfundishaye kupata faida.

Isy 48:17
MUNGU hakufunsidhi tu kuhubiri au kuimba bali pia ukufundisha na upanga FIKRA zako ili zipate kujua MUNGU ndiye akupaye faida

FIKRA lazima zipate msaada wa kufundishwa jinsi ya kupata faida

Pata tofauti sana kati ya kufundishwa kupata faida na kufundishwa Biashara. Ni sawa na ilivyo tofauti kati ya kufundishwa kufaulu mtihani darasani na kufundishwa juu ya kufaulu mtihani wa kimaisha

Maana si kila mtu aliyeko darasani atafaulu maisha, na si kila afanyaye Biashara atapata faida..lazima ujifunze kuvuka hapa

MAENEO MUHIMU YA KUTAKIWA KUBADILIKA

1). Weka FIKRA zako zikubali MUNGU ndiye anayekufundisha kupata faida

Watu wengi wakikwama kiroho ukimbilia kanisani ila uchumi wao ukikwama huwaoni kanisani ukimbilia Benki, sasa sisemi Benki ni mbaya au usiende Benki ila wanasahau kuwa

ROHO MTAKATIFU ni mwalimu mzuri sana wa kukugundisha ujasiriamali wenye kupata faida

2). Lipa Deni
Elisha alimwambia Mama mjane ....kauze kisha lipa deni....

Alikuwa anatafuta kitu gani?
Alikuwa anapandikiza nidhamu za kutumia fedha ambazo MUNGU amekupa kwa sababu zake alizokupa au ulizomwomba tena kwa mwongozo wake!

Mama mjane alikwenda kutaka msaada wa watoto wake kitokuchukuliwa watumwa(Alitaka kupata fedha za kuwakomboa watoto wake)

Hakuwa na FIKRA zilizojengeka kulipa deni maana Biblia haituonyeshi aliwahi kukopa. Kama huna FIKRA za kukopa huwezi ukawa na FIKRA za kulipa deni.

Mama mjane alikabidhiwa matumizi ya fedha ktk maeneo haya
Kulipa deni
Gharama za kwake na zile za baadaye
Gharama za watoto na za wakati ule wa baadaye
Kuhakikisha ya kwamba amalizi faida lazima abaki na mtaji.

Je unamwomba MUNGU pesa kwa ajili ya nini au kwa ajili gani?
Kumbuka pesa uyumbisha mawazo na kujikuta watumia nje ya lile kusudio

Ukikorofisha hapo MUNGU ukaa pembeni. FIKRA zinahitaji nidhamu kwenye matumizi ya pesa. Kama MUNGU anakupa kwa ajili ya kitu fulani hakikisha unaielekezea hyo pesa kwenye hicho kitu.

Tofauti na hapo utaona ROHO MTAKATIFU anakuhimiza TOBA

Mith 13:22
Watu wengi wana FIKRA za kujitazama wenyewe tu kwenye upande wa pesa wanajikuta kusahau kuwa wana familia na watoto!

Biblia inatuhimiza kuweka akiba mpaka za wajukuu!

Usitazame kukwama kwa mme/mke wako ama wazazi wako, usifike mahali hata pa kuwakasirikia badili FIKRA zako ili wewe uvuke hapo kisha mrushie kamba naye atoke hapo oooh hallelujah Hallelujah







HOME WORK
Orodhesha madeni yako

Zab 37:21
Umuhimu wa kuorodhesha madeni

Usipolipa mikopo MUNGU haji kukupigania katika haki zako.
Unapoteza haki katika haki
Mikopo isiyolipwa ugeuka deni
Deni ubeba vitu (rehani) ili akili zako ziamke. Na baada ya kutaka kuja kuvichukua ndipo akili zako zitaamka
Si kila ambaye anashindwa kulipa deni hana hela bali hana mpangilio mzuri wa matumizi na ulipaji

Yer 22:21
Si kwamba hapendi kusikia bali hataki kusikia maana yake hataki kutekeleza alichoambiwa

Gharama kubwa ya kutokufaulu mipango yako ni kupoteza utulivu wa MUNGU kukusemesha

Wengi wakisha kopa kwenye kulipa ulipa nusu na nusu wanaweka mfukoni wanasahau MUNGU ndiye aliwafundisha kupata faida na au walipewa kibali cha kupata mkopo

Usije ukasahau na kusema huu utajiri ni nguvu zangu wakati ni MUNGU ndiye aliyekupa nguvu za kupata utajiri



No comments:

Post a Comment

Makala nyingine

IMPORTANCE OF OUR TESTIMONIES IN THE CHURCH

Mathayo 8:1-4 Naye aliposhuka mlimani, makutano mengi walimfuata.  Na tazama, akaja mtu mwenye ukoma akamsujudia, akisema, Bwana, u...