Thursday, September 29, 2016

SOMO LA FIKRA PART 5.

.
UNAFIKIRI KWANINI MUNGU ALILETA SADAKA

Si kwamba ana shida na pesa yako
Lengo la kwanza lilikuwa kutumia sadaka kukutengenezea FIKRA sahihi ndani yako
Tazama maana ya
Malimbuko=MUNGU anataka umfikirie yeye kwanza
Zaka ya kwanza=MUNGU anataka kupewa heshima ktk maisha yako

Watu wengi kwenye kipindi kigumu na chenye kibano wako tayari kutafuta hela kulipa Benki lakini si kwa MUNGU. Kwa MUNGU excuses zitakuwa nyingi sana na hata kusema "MUNGU we si unajua nilivyobanwa"

MUNGU hana maana wala hataki kukufirisi bali anataka kukutengenezea FIKRA zenye Nidhamu

Jifunze kumpa MUNGU 100% naye anakurudishia 100%

Muulize MUNGU kwanza kwenye kila kitu, ratiba zako, muda wako na mambo yako mkabidhi na mfikirie MUNGU kwanza

Usitamani kuiga maisha na FIKRA za mtu mwingine hakikisha MUNGU anakupa mbinu za kujenga FIKRA za kwako mwenyewe.

FIKRA zenye kujenga nidhamu ndani yako.zitakufanya utende haki wala hazitakupeleka kwenye kupokea rushwa

FIKRA hizi zitakuwekea unyenyekevu ndani yako, kujishusha na kujifunza kutoka kwa wengine

Usijaribu ku copy na ku paste kutoka kwa mtu mwingine BWANA atakupa mikakati sahihi ndani yako

HATUA AMBAZO UNAHITAJI KUZIFUATA KAMA UNATAKA KUTUMIA FIKRA ZIKUSOGEZE KIMAISHA.....[Zinaendelea...]

2Tasmini kufikiri kwako ili uweze kushirikiana na MUNGU anapotaka kukusaidia kimaisha.

Haifanani na hatua ya kwanza
Tafsiri nyingine ni kama ifuatavyo Mith 23:7
....aonavyo nafsini mwake...
Biblia haisemi aonacho bali aonavyo si afikiricho bali afikirivyo si anachotafakari bali anavyotafakari

Kumbuka alichosema YESU kwenye Math 13:13-14

Biblia haizungumzi tu juu ya aonavyo, bali anaonavyo anachoona
Kinachomsaidia kuona anachoona si swala la kufikiri bali jinsi ya kufikiri
Ni kitu gani kinachokusukuma kufikiri na kuja na jibu ulilonalo?

Kumbuka habari ya wale wapelelezi 12
10:- waliona majitu
2:- waliona chakula

Walitazama lakini hawakuona
Ndivyo ilivyo wengi usoma NENO kumbe hawasomi, wengi usikiliza kumbe hawasikilizi

Shida ni nini??
Nafsi=FIKRA zimefungwa!

Rum 1:28
Ufahamu ulioko ktk nafsi ni tofauti na ufahamu ulioko ktk roho
Unasema najuaje...ndiyo maana anazungumzia.habari za akili hapa...na akili haipo rohoni bali kwenye nafsi
Ukimkataa MUNGU kwenye fahamu zako ama kumuacha, basi utafuata akili zisizofaa, zako na za wengine!
Kwa sababu hyo utajikuta unafanya mambo usiyotaka kufanya
Kwa lugha rahisi kumwacha MUNGU huwezi tembea ktk mpango wake juu yako
Ukimkubali KRISTO hawezi kukuacha utembee nje ya mpango wa MUNGU

Akili zisizofaa ni nini
Unachotakiwa wewe kukijua/kukifuata wewe kama wewe!

Na wala si maana yake kwamba ni akili mbaya

Maana yake ni FIKRA ambazo kwa mtu mwingine si zake mwingine ni zake. Mfano mfanyabiashara astahili kumwona mfanyakazi ofisini anafanya kisicho sawa na vivyohivyo mfanyakazi kumtazama mfanyabiashara kuwa amepotea!

Ukiruhusu na kukubali MUNGU akutawalate anakupa FIKRA za kusimama alipokusudia hata kama akikuletea washauri watakushauri ktk FIKRA za MUNGU juu yako na wala hawatatumia akili mbaya

MUNGU anataka kutusaidia ili tuishi maisha ya kiwango cha Ki-Agano maana huko ndiko kwenye kusudi la kila mmoja!
Viwango vyetu vya maisha vimefungwa ktk Agano(kwa sasa twatumia Agano jipya ila tusisahau na kuliacha maana ktk lile la kale MUNGU alishaweka maagano pia)

Hebr 8:8-10
Hebr 4:12-13
MUNGU akitaka kukufanikisha utuma NENO ktk nafsi yako(FIKRA) ili nafsi iweze kutafsiri lile NENO kati ya roho na mwili

MUNGU anapotuma NENO lile NENO lina uwezo wa kutambua mawazo na makusudi ya nafsi

NENO ukagua aina ya FIKRA au mawazo uliyonayo ktk kuendesha maisha yako.

Zab 117:19-20
Ukimlilia MUNGU utuma NENO lake na NENO ukagua mambo haya:-
1Aina ya FIKRA na akili unazotumia
2Pia imsaidie maamuzi ndani yake aina gani ya akili(FIKRA) unazihitaji mahali ulipo
3NENO la MUNGU linampa MUNGU nafasi ya uhalali/kibali kwako

Isaya 55:8-11
kuna pointi kama 4 hapa muhimu uzidake
WAZO:- MUNGU utuma wazo ndani ya mtu
NJIA:- Ukisha tafakari wazo ukupa njia(MIKAKATI)
MVUA:- Uachiliwa mvua kuzidi kunyeshea listawi na kukua hilo wazo
NENO:- kwa hiyo NENO ufanikiwa hakika

Usishtuke litakapokuja wazo tofauti na ulilonalo hyo ni ishara ya kuambiwa jipange ili utoke mahali ulipo

Kumbuka kama nafsi yako haitakuwa tayari kupokea hata YESU asimame mbele yako utamgomea tu, sababu ni nini mafundisho tunayopokea. Yoh 8:31-59

Ukikataa msaada wa maelekezo yake utakuwa na maisha ya kuishi jangwani tu(maisha ya mzunguko tu usijue ushike nini uache nini) na mbinguni ila jiulize Airport yako itakuwa wapi? Jangwani au Kaanani?







TURUDI KWA MAMA MJANE TUJIFUNZE KITU

2Falm 4:1-7

MASWALI AMBAYO YANAWEZA KUKUSAIDIA KATIKA KUTATHIMINI KWAKO

1Je ninajua ni aina gani ya masaada ninaohuitaji ili niwe na maisha mazuri kuliko niliyonayo sasa?

Swali hili tunalipata kwa mama mjane baada ya kujieleza Elisha akamuuliza swali nikufanyie nini

Mama hakujibu lile swali hakusema anahitaji msaada gani bali alipekeka ripoti ya hali yake ya maisha aliyokuwa nayo baada ya kufa mumewe.

Alishindwa kujibu yawezekana kwa mambo haya:-
-FIKRA zake hazikuwa na jibu ya swali hilo
-FIKRA zake zilikuwa zimeishiwa mawazo ya kumtoa ktk shida hyo
-FIKRA zake zilikuwa zinataka kutua mzigo bila kujua atabebeshwa mzigo wa lile swali unataka nikufanyie nini

MUHIMU SANA KUFAHAMU SIRI ZILIZOKO KTK MASWALI YA NAMNA HIYO
Kushindwa kujibu maswali/swali la Elisha maana yake au inaonyesha
Matatizo yake yalikula muda wake wa kufikiri kiasi ambacho hakubakiza muda wa kufikiria jibu

Muda wako ukiliwa na kukatawaliwa na matatizo huwezi fanya maamuzi, unapigwa bumbuazi huwezi pata hata wazo la kufanya ndani yako. Utabaki kukaa na hasira na huzuni

Usikubali mazingira yakuwekee ngome inayokwamisha/kuzuia kufikiri kwako zaidi ya mawazo uliyonayo sasa

Mwz 26:1-14
MUNGU aliisemesha FIKRA yake isitazame mazingira bali aangalie Agano

2Kor 10:3-5
Shetani upambana na kuvuruga sana FIKRA ndani ya mtu

2Kor 11:3
Unapoona mapambano ya FIKRA ndani yako usiruhusu kabisa matatizo kuyaona ni makubwa kuliko NENO ndani yako

Shetani uleta hila ndani ya mtu kwenye FIKRA ili kukuvuruga

HILA MAANA YAKE NINI
1Wazo linalokuja kukuzuia uwezo wa FIKRA zako kupokea cha MUNGU na kama ulikuwa umekipokea unakikataa

2Ukweli+Uongo=Usipovitenga jibu ni Uongo. Jiulize pale Edeni mti wa mema+mabaya=mabaya

Cheki wazo linapokuja ndani yako ROHO MTAKATIFU anasemaje? Kama si la kusudi la MUNGU utakosa amani, utapata huzuni(maana yake change your mindset fanya TOBA)
Uhitaji kufikiria mtu anayekuja na wazo fikiria na sikia wazo la MUNGU pekee

Ukikosa amani usiendelee na hilo wazo
-Cheki ndoto unazoota kama ni
Nyoka=kuna hila inakuja kuvuruga FIKRA zako kama kakung'ata ujue kaacha sumu na kama la jua kaacha hofu!

Ngome=kuna kizuizi umefungiwa ndani, ulitakiwa kutoka

Stendi=Kufikiri kwako kumekwama

Unapoomba ombea sumu kuondoka na kama kuna roho ya kufuatilia utekelezaji bado ipo kemea

*Teka kila nyara na kila FIKRA=zilizimishe kufikiri ki FLAME na KI AGANO






HOME WORK
YESU akisimama mbele yako leo akikusemesha unataka nikufanyie nini utajibu nini??

Ukishindwa kujibu ni wazi kufikiri kwako kumekwama!

KWANINI MUNGU ANAULIZA MASWALI HAYA
1Kumlazimisha aliye uliza alazimishe FIKRA zake kufikiri mahali zilipokwama

2Anatafuta uhalali/kibali cha kuingilia kufikiri kwako maana anaweza kuja na wazo jipya ukakataa


No comments:

Post a Comment

Makala nyingine

IMPORTANCE OF OUR TESTIMONIES IN THE CHURCH

Mathayo 8:1-4 Naye aliposhuka mlimani, makutano mengi walimfuata.  Na tazama, akaja mtu mwenye ukoma akamsujudia, akisema, Bwana, u...