Hesabu 14 :6-9
6 Na
Yoshua mwana wa Nuni, na Kalebu mwana wa Yefune, waliokuwa miongoni mwao
walioipeleleza nchi, wakararua nguo zao;
7 wakanena
na mkutano wote wa wana wa Israeli wakasema, Nchi ile tuliyopita kati yake ili
kuipeleleza, ni nchi njema mno ya ajabu.
8 Ikiwa
Bwana anatufurahia, atatuingiza katika nchi hii atupe iwe yetu, nayo ni nchi
yenye wingi wa maziwa na asali.
9 Lakini
msimwasi Bwana, wala msiwaogope wale wenyeji wa nchi, maana wao ni chakula kwetu;
uvuli uliokuwa juu yao umeondolewa, naye Bwana yu pamoja nasi; msiwaogope.
JOSHUA
14:10-14
10 Sasa
basi, angalia, yeye Bwana ameniweka hai, kama alivyosema, miaka hii arobaini na
mitano, tangu wakati huo Bwana alipomwambia Musa neno hilo, wakati Israeli
waliokuwa wakienenda barani; na sasa tazama, hivi leo nimepata miaka themanini
na mitano umri wangu.
11 Hata
sasa mimi nina nguvu zangu hivi leo kama nilivyokuwa siku hiyo Musa
aliyonituma; kama nguvu zangu zilivyokuwa wakati huo, na nguvu zangu ndivyo zilivyo
sasa, kwa vita na kwa kutoka nje na kuingia ndani.
12 Basi
sasa unipe mlima huu, ambao Bwana alinena habari zake siku hiyo; kwani wewe
ulisikia siku hiyo jinsi Waanaki walivyokuwa huko, na miji ilivyokuwa mikubwa
yenye boma; yumkini yeye Bwana atakuwa pamoja nami, nami nitawafukuza watoke
nje, kama Bwana alivyonena.
13 Yoshua
akambarikia, akampa Kalebu, huyo mwana wa Yefune, Hebroni kuwa urithi wake.
14 Kwa
hiyo Hebroni ukawa urithi wa Kalebu, mwana wa Yefune, Mkenizi, hata leo; kwa
sababu alimwandama Bwana, Mungu wa Israeli, kwa utimilifu.
·
Caleb akiwa takriban miaka 40
alimfurahisha Mungu kwa kuwa na imani wao watachukua nchi/ardhi.......
·
Caleb
alikuwa ni miongoni kati ya spy wapelelezi 12 waliochaguliwa katika kila
kabila la Israel
·
Kwakuwa alichaguliwa kuwa mmoja wa
wapepelezi basi caleb alikuwa ni mtu wa
heshima katika kabila lake ndo maana alichagulia
Calebu
alikuwa ni mtu jamii ya wakenizi
Yoshua 14:6
[6] Wakati huo wana wa
Yuda walimwendea Yoshua hapo Gilgali; na Kalebu, mwana wa Yefune, huyo Mkenizi,
akamwambia, Wewe wajua hilo neno BWANA alilomwambia Musa, huyo mtu wa Mungu,
katika habari zangu, na katika habari zako wewe, tulipokuwa katika
Kadesh-barnea.
Mwanzo 15:18-19, 21
[18] Siku ile BWANA
akafanya agano na Abramu, akasema, Uzao wako nimewapa nchi hii, kutoka mto wa
Misri mpaka huo mto mkubwa, mto Frati, [19] Mkeni, na Mkenizi, na Mkadmoni,
[21] na Mwamori, na Mkanaani, na Mgirgashi, na Myebusi.
Mwanzo 36:8-11
[8] Esau akakaa katika
mlima Seiri, Esau ndiye Edomu. [9] Hivi ni vizazi vya Esau, baba ya Edomu
katika mlima Seiri. [10] Haya ndiyo
majina ya wana wa Esau; Elifazi, mwana wa Ada mkewe Esau. Reueli, mwana wa
Basemathi, mkewe Esau. [11] Na wana wa Elifazi, ni Temani na Omari, na Sefo, na
Gatamu, na Kenazi.
SIFA
YA KALEBU
Ø Alikuwa
ni mtu jasiri Alikubali kwenda kuperereza nchi ambayo ni hatari na ngumu....
2 Timotheo 1:7
Maana Mungu hakutupa
roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi.
Ø Alikuwa ni mtu wa kujitoa Kufanana kwake anafananishwa
na paulo
2 Timotheo 4:6-8
Kwa maana, mimi sasa
namiminwa kama tambiko, na wakati wa kuondoka kwangu umefika. [7] Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo
nimeumaliza, Imani nimeilinda; [8] baada
ya hayo nimewekewa taji la haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa
siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake.
Ø Calebu alikuwa mtu wa imani na alimuamini
Mungu Alisema " Mungu yupo pamoja nasi tusiwaogope "
Hesabu 14:9
Lakini msimwasi BWANA,
wala msiwaogope wale wenyeji wa nchi, maana wao ni chakula kwetu; kinga
iliyokuwa juu yao imeondolewa, naye BWANA yuko pamoja nasi; msiwaogope.
Warumi 8:31
Basi, tuseme nini juu ya
hayo? Mungu akiwapo upande wetu, ni nani awezaye kutupinga?
Ø Calebu
alimhofu Mungu dhidi ya watu walio mzunguka
Alikubali kuwa watu
wale ni hodari na niwakubwa lakini alisema Mungu yupo pamoja nasi.
IMANI
YA CALEBU
Caleb aliweza kumfurahisha Mungu kutokana na imani
yake.
Mlima Hebron ulikuwa
unamilikiwa na wanaak. Hawa walikuwa ni watu wenye size kubwa . Walikuwa ni
watu wanaofahamika kuwa ni mashujaa kutokana na uhodari wao.
Calebu alimwambia
joshua nipe mlima huu nitawaondoa majitu
katika mlima huu,
Kwa Calebu ule mlima
ulikuwa ni changamoto hakuogopa chochote
Vitu
unavyo hitaji ili uweze kumiliki na
kuupanda mlima.
1.
Unaitaji kutiwa moyo/nguvu
Calebu alikubali ile
kazi lakini ilikuwa ni ngumu . Ile kazi ilikuwa na uwoga mwingi na ilikuwa unafanya ukiwa na pressure kubwa.
.Kutiwa moyo hakuondoi
sura ya kuogopa bali inakupa kufanya kitu sahihi katika hali yako ya uwoga
,Hakuna mlima unaoweza kupata kama hutotiwa moyo.
Luka 22:43
Malaika kutoka mbinguni akamtokea akamtia nguvu.
Hii tunapata pale Yesu
alipotaka kwenda Yerusalem alilia kwa uchungu mpaka malaika wakaja kumtia
nguvu. Maana kile kikombe kilikuwa ni kikubwa .
Kuna wakati
unaweza taka kufanya kitu cha tofauti
lakini ndani yako unapopata woga
unaitaji mtu wa kukutia nguvu.
Yamkini unataka kufungua campuni, au biashara, usiogope yupo roho mtakatifu ambaye atakutia
moyo . ... na kukutia nguvu
Kuna watu ambao
wanapenda kufanya mambo kivyao vyao
. Na hawataki kutiwa moyo na wenzao
wanahisi wataonekana wazaifu. Hapana
kwenye kila hali unaitaji kutiwa moyo ..
2. Unatakiwa
uanze kufanya jambo
Kuanza ni kupiga
hatua ya uwajibikaji calebu ndo wa kwanza kusema "tukawaondoshe majitu" na ni calebu
aliye mpa mpango joshua nataka kwenda kuwaondoa
wana wa anak katika mlima hebron. Huwez kuyashinda majalibu kama usipo piga hatua ya kwanza. Watu wengi wanashindwa kusonga mbele kwa
sababu hawawez kupiga hatua .Hawataki kuwa waanzilishi wa jambo.
Ni kweli kuanzisha
jambo kuna gharama lakini gharama zake
hazina maumivu ukisha fanikiwa.
Waebrania
11:8
Kwa
imani Abrahamu alipoitwa aliitika, atoke aende mahali pale atakapopapata kuwa
urithi; akatoka asijue aendako.
Ibrahimu aliambiwa na
Mungu aache watu wake na kumfuata Mungu,
ni kweli ilimuuma lakini lengo la Mungu ni kumbariki Ilikuwa ngumu kwa
mke wake Sarah's lakini kwasababu ibrahimu alikuwa ni different. Alikubali......
Kutoka 3:3
Musa akasema, Nitageuka sasa niende nione kioja hiki, kwa nini
kichaka hiki hakiteketei.
Moses aliona kichaka
kinawaka moto akachukua hatua ya kukitazama
ndipo Bwana akaamua kuongea nae . Baada ya ile hatua Musa akawa mkombozi
wa wana wa Israel. Ilikuwa ngumu kwake kwenda kuwakomboa lakini mkono Bwana
ulikuwa juu yake.
Danieli 9:2
katika
mwaka wa kwanza wa kutawala kwake, mimi Danieli, kwa kuvisoma vitabu, nilifahamu
hesabu ya miaka, ambayo neno la BWANA lilimjia Yeremia nabii, ya kuutimiza ukiwa wa
Yerusalemu, yaani, miaka sabini.
Daniel alichukua hatua
ya kusoma vitabu akajua miaka ya kuishi utumwani imeisha ,Mungu amekupa akili
na maarifa ili uweze kufanya maamuzi .
Ukipiga hatua ya kufanya jambo mungu
atakupa bonus .
3. Unatakiwa kuwa na nia moja
Mithali 4 :25
Macho yako yatazame mbele, Na kope zako zitazame mbele yako sawasawa.
Kwenye kila jambo
ambalo ni mapenzi ya Mungu, unatakiwa ku focus na kujitoa kwa moyo na akili ili
ulifanikishe, ndicho caleb ambacho alikifanya
, tangu akiwa na 40 yrs mpaka 80
yrs aliwaza kupata ile ahadi aliyo pewa na musa.
4. Unatakiwa ufanye kazi kwa moyo wako wote
Mfalme hezekia alisema kwenye neno lake alifanya kazi kwenye nyumba ya Bwana alifanya kwa moyo wote
2 wafalme 20:1-6 Siku
hizo Hezekia akaugua, akawa katika hatari ya kufa. Isaya, nabii, mwana wa
Amozi, akamjia akamwambia, Bwana asema hivi, Tengeza akasema,
3 Nakusihi,
Bwana, ukumbuke sasa, jinsi nilivyokwenda mbele zako katika kweli na kwa moyo
mkamilifu, na kutenda yaliyo mema machoni pako. Hezekia akalia sana sana.mambo
ya nyumba yako; maana utakufa, wala hutapona.
2 Basi
Hezekia akajigeuza, akaelekeza uso wake ukutani, akamwomba Bwana
Kalebu nae alifanya
hivyo hivyo alitembea na Mungu kwa moyo wake wote
5. Unatakiwa uwe na uvumilivu
Kalebu alisubri mpaka
ulipofika wakati sahihi wa Mungu , ndipo akamkumbusha Joshua ahadi aliyopewa na mtumishi musa,
Isaya 40 : 31 bali wao wamngojeao Bwana watapata
nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka;
watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia
6. Usiache kukua /kuongezeka
Mwanzo 1:28a
Mungu
akamwambia, Mimi ni Mungu Mwenyezi, uzidi ukaongezeke.
Katikati ya changamoto
na mlima unaoutaka usiache kukua na kuongezeka . jitahidi sana kuongezeka ki fikra, elimu na ki
maendeleo kwasababu wakati ukifika wa kupanda kwenye mlima unatakiwa usikose,
yamkini mlima wako ni biashara, basi kabla ujafungua hiyo biashara inabidi
upate maarifa mengi kuhusu biashara,

No comments:
Post a Comment