Monday, November 17, 2025

HAPO SIO SEHEMU YA KUPUMZIKA

 Mika 2:10 BHN
[10] Inukeni mwende zenu! Hapa hamna tena pa kupumzika! Kwa utovu wenu wa uaminifu maangamizi makubwa yanawangojea!


Kuna hali katika maisha ya vijana ambayo inamfanya mtu kurizika kiwango alicho nacho. 

Si vibaya , lakini biblia inatukumbusha kuwa katika hali yoyote ya mafanikio hatutakiwi kurizika wala kupumzika...

Duniani tunapita lakini pia tuna assignment kubwa ya kufanya   
1. Ufalme wa Mungu 
2. Maisha ya kila siku 

Chochote kilicho chema , tunachopata au tunachotenda ni kwa ajili ya ufalme wa Mungu.
Na uzuri Yesu alisema tuende ulimwenguni kote kuhubiri/kutangaza/kushuhudia mambo anayofanya kwenye maisha yetu .
Hiyo inaonesha kuwa hatutakiwi kupumzika maana tukipumzika tutadumaa kiroho, kiakili, na kimtazamo
Biblia ya NIV anasema

Micah 2:10 NIV
[10] Get up, go away! For this is not your resting place, because it is defiled, it is ruined, beyond all remedy.

Yesu anatamani kila siku tuwe na kazi ya kufanya kwa ajili ya ufalme wa Mungu. 

Kama kwenye biashara anatamani biashara iwe kubwa ili wateja waongezeke na washuhudie kuwa wewe ni mtumishi wa Mungu 

Kama kwenye siasa , anatamani uwe kiongozi mkubwa sana ili Jina lake litambulike kupitia wewe

Kama ni ndoa , anatamani uwe mke au mume mzuri ili jamii iliyo kuzunguka waone maisha ya Yesu ndani Yenu.
Why wana wa Israel waliambiwa Na Mungu imetosha kuzunguka mlima ule 

Kum 2:3
Mlivyouzunguka mlima huu vyatosha; geukeni upande wa kaskazini.

Kwa sababu anajua mwanadamu huwa anachoka na kudumaa akiwa sehemu moja...
So aliwaonyesha uelekeo ili wa Destiny yao ya maisha...

So Mungu akisema kuwa hiyo sio sehemu kupumzika kwako basi lazima akuonyeshe uelekeo wa kwenda.
Kuna nabii mmoja aliitwa eliya , malaika alimwamsha na kumpa chakula, na akamwambia ongeza chakula kwa sababu safari yako bado ni ndefu 

1 Kings 19:7 NIV
[7] The angel of the Lord came back a second time and touched him and said, “Get up and eat, for the journey is too much for you.”


1 Wafalme 19:7 SRUV
[7] Malaika wa BWANA akamwendea mara ya pili, akamgusa, akasema, Inuka, ule; maana safari hii ni kubwa mno kwako.
Kwa kawaida na akili zetu tunaweza sema tumefika lakini Mungu anasema bado safar ni ndefu..
Tunaitaji kuomba sana, kula neno la Mungu, kusoma , kujifunza hekima zote za dunia ambazo zitatusaidia kwenye maisha...

Yamkini hii safar yako ya maisha ni Ngumu lakini usikate tamaa, jiandae kwa ajili ya kizazi chako cha baadae.

Don't rest and don't give up...

Amen

Tuesday, September 2, 2025

SAFARI YAKO BADO NDEFU


1 Wafalme 19:7
[7] Malaika wa BWANA akamwendea mara ya pili, akamgusa, akasema, Inuka, ule; maana safari hii ni kubwa mno kwako.
English version 
1 Kings 19:7 NIV
[7] The angel of the Lord came back a second time and touched him and said, “Get up and eat, for the journey is too much for you.”

Utangulizi 
Upendo wa Mungu ni mkubwa kwetu, inapeleka kutuhimiza kusoma neno lake sana. 
Hatusomi neno kwa sababu  ni menyu yetu ya maisha, bali tunalisoma kwa sababu safari yetu ni ndefu na ni kubwa mno...

When God say eat, ana maanisha kuwa kila siku unatakiwa ujiandae kwa shughuli zijazo , word of God sometimes linakuja kama wazo au taarifa...., there is information you need to meditate (eat) ili uweze kufanya decision in your future journey.

1.Wazo
So sometimes Gods use sound minds to tells us about future, unakuta mara nyingi kitu kinajirudia rudia akili. Tambua hapo Mungu anasema na wewe kuwa hilo wazo lichambue au likatekate  (meaditation), litafune, mpaka upate strategies ...., 
Tunajua kuwa chakula kikiwa kwenye kinywa lazima tutafune, na lengo  la kutafuna ni kusaidia mmeng'enyo wa chakula uwe kwa urahisi, kwaiyo tunapo chambua wazo la Mungu ndo tunapata urahisi wa kufanikisha safari  yetu ya maisha.

So Mungu ameweka safari ndefu ya maisha katika mikono yetu ameweka utajiri, nguvu, hekima lakini , sisi wenyewe ndo huwa tunataka tusikifike nchi ya ahadi kwasababu  hatuna maarifa mengi....
Biblia inasema kwenye kitabu cha daniel  ( daniel 9)
[2] katika mwaka wa kwanza wa kutawala kwake, mimi Danieli, kwa kuvisoma vitabu, nilifahamu hesabu ya miaka, ambayo neno la BWANA lilimjia Yeremia nabii, ya kuutimiza ukiwa wa Yerusalemu, yaani, miaka sabini.....

Daniel kwa kuvisoma vitabu alifahamu hesabu ya miaka/siku za kukaa utumwani kwaiyo alijua na aliweza kufanya maamuzi ambayo yaliwasaidia wana wa Israel kurudi katika nchi yao.

 Hii inatuhimiza kuwa katika  mafanikio ambayo unayataka  yapo kwenye (vitabu) mawazo ya watu yaliyo kwenye karatasi, 

Ni juhudi zetu kama wana wa Mungu kusoma na kuchambua ili tupate kufanikiwa kwenye mambo yetu. 

Mfano unataka kuwa mfanyabiashara,  kuna hekima nyingi ambazo watumishi wa Mungu kupitia sauti ya Mungu wameweka kwenye vitabu... so ni wewe ndiye unatakiwa kuongeza juhudi za kujifunza

To be continue......

Sunday, August 11, 2024

NIPE MLIMA HUU (Give me that mountain)

 



Hesabu 14 :6-9

Na Yoshua mwana wa Nuni, na Kalebu mwana wa Yefune, waliokuwa miongoni mwao walioipeleleza nchi, wakararua nguo zao;
wakanena na mkutano wote wa wana wa Israeli wakasema, Nchi ile tuliyopita kati yake ili kuipeleleza, ni nchi njema mno ya ajabu.
Ikiwa Bwana anatufurahia, atatuingiza katika nchi hii atupe iwe yetu, nayo ni nchi yenye wingi wa maziwa na asali.
Lakini msimwasi Bwana, wala msiwaogope wale wenyeji wa nchi, maana wao ni chakula kwetu; uvuli uliokuwa juu yao umeondolewa, naye Bwana yu pamoja nasi; msiwaogope.

JOSHUA 14:10-14

10 Sasa basi, angalia, yeye Bwana ameniweka hai, kama alivyosema, miaka hii arobaini na mitano, tangu wakati huo Bwana alipomwambia Musa neno hilo, wakati Israeli waliokuwa wakienenda barani; na sasa tazama, hivi leo nimepata miaka themanini na mitano umri wangu.
11 Hata sasa mimi nina nguvu zangu hivi leo kama nilivyokuwa siku hiyo Musa aliyonituma; kama nguvu zangu zilivyokuwa wakati huo, na nguvu zangu ndivyo zilivyo sasa, kwa vita na kwa kutoka nje na kuingia ndani.
12 Basi sasa unipe mlima huu, ambao Bwana alinena habari zake siku hiyo; kwani wewe ulisikia siku hiyo jinsi Waanaki walivyokuwa huko, na miji ilivyokuwa mikubwa yenye boma; yumkini yeye Bwana atakuwa pamoja nami, nami nitawafukuza watoke nje, kama Bwana alivyonena.
13 Yoshua akambarikia, akampa Kalebu, huyo mwana wa Yefune, Hebroni kuwa urithi wake.
14 Kwa hiyo Hebroni ukawa urithi wa Kalebu, mwana wa Yefune, Mkenizi, hata leo; kwa sababu alimwandama Bwana, Mungu wa Israeli, kwa utimilifu.

·        Caleb akiwa takriban miaka 40 alimfurahisha Mungu kwa kuwa na imani wao watachukua nchi/ardhi.......

·        Caleb  alikuwa ni miongoni kati ya spy wapelelezi 12 waliochaguliwa katika kila kabila la Israel

·        Kwakuwa alichaguliwa kuwa mmoja wa wapepelezi basi caleb  alikuwa ni mtu wa heshima katika kabila lake ndo maana alichagulia

Calebu alikuwa ni mtu jamii ya  wakenizi

Yoshua 14:6

[6]  Wakati huo wana wa Yuda walimwendea Yoshua hapo Gilgali; na Kalebu, mwana wa Yefune, huyo Mkenizi, akamwambia, Wewe wajua hilo neno BWANA alilomwambia Musa, huyo mtu wa Mungu, katika habari zangu, na katika habari zako wewe, tulipokuwa katika Kadesh-barnea.

Mwanzo 15:18-19, 21

[18]  Siku ile BWANA akafanya agano na Abramu, akasema, Uzao wako nimewapa nchi hii, kutoka mto wa Misri mpaka huo mto mkubwa, mto Frati, [19] Mkeni, na Mkenizi, na Mkadmoni, [21] na Mwamori, na Mkanaani, na Mgirgashi, na Myebusi.

Mwanzo 36:8-11

[8]  Esau akakaa katika mlima Seiri, Esau ndiye Edomu. [9] Hivi ni vizazi vya Esau, baba ya Edomu katika mlima Seiri. [10]  Haya ndiyo majina ya wana wa Esau; Elifazi, mwana wa Ada mkewe Esau. Reueli, mwana wa Basemathi, mkewe Esau. [11] Na wana wa Elifazi, ni Temani na Omari, na Sefo, na Gatamu, na Kenazi.

 

 

SIFA YA KALEBU

Ø Alikuwa ni mtu jasiri Alikubali kwenda kuperereza nchi ambayo ni hatari na ngumu....

2 Timotheo 1:7

  Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi.

Ø   Alikuwa ni mtu wa kujitoa Kufanana kwake anafananishwa na paulo

2 Timotheo 4:6-8

  Kwa maana, mimi sasa namiminwa kama tambiko, na wakati wa kuondoka kwangu umefika. [7]  Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda; [8]  baada ya hayo nimewekewa taji la haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake.

 

 

 

Ø  Calebu alikuwa mtu wa imani na alimuamini Mungu Alisema " Mungu yupo pamoja nasi tusiwaogope "

 

Hesabu 14:9

 Lakini msimwasi BWANA, wala msiwaogope wale wenyeji wa nchi, maana wao ni chakula kwetu; kinga iliyokuwa juu yao imeondolewa, naye BWANA yuko pamoja nasi; msiwaogope.

Warumi 8:31

 Basi, tuseme nini juu ya hayo? Mungu akiwapo upande wetu, ni nani awezaye kutupinga?

Ø Calebu alimhofu Mungu dhidi ya watu walio mzunguka

Alikubali kuwa watu wale ni hodari na niwakubwa lakini alisema Mungu yupo pamoja nasi.

 

IMANI YA CALEBU

Caleb  aliweza kumfurahisha Mungu kutokana na imani yake.

Mlima Hebron ulikuwa unamilikiwa na wanaak. Hawa walikuwa ni watu wenye size kubwa . Walikuwa ni watu wanaofahamika kuwa ni mashujaa kutokana na uhodari wao.

Calebu alimwambia joshua nipe mlima huu  nitawaondoa majitu katika mlima huu,

Kwa Calebu ule mlima ulikuwa ni changamoto hakuogopa chochote

Vitu unavyo hitaji  ili uweze kumiliki na kuupanda mlima.

1. Unaitaji kutiwa moyo/nguvu

Calebu alikubali ile kazi lakini ilikuwa ni ngumu . Ile kazi ilikuwa na uwoga mwingi na  ilikuwa unafanya ukiwa na pressure kubwa.

.Kutiwa moyo hakuondoi sura ya kuogopa bali  inakupa  kufanya kitu sahihi katika hali yako ya uwoga ,Hakuna mlima unaoweza kupata kama hutotiwa moyo.

 

Luka 22:43

Malaika kutoka mbinguni akamtokea akamtia nguvu.

Hii tunapata pale Yesu alipotaka kwenda Yerusalem alilia kwa uchungu mpaka malaika wakaja kumtia nguvu. Maana kile kikombe kilikuwa ni kikubwa .

Kuna wakati unaweza  taka kufanya kitu cha tofauti lakini ndani yako unapopata woga  unaitaji  mtu wa kukutia nguvu.

Yamkini  unataka kufungua campuni, au biashara,  usiogope yupo roho mtakatifu ambaye atakutia moyo . ... na kukutia nguvu

Kuna watu ambao wanapenda kufanya mambo  kivyao vyao .  Na hawataki kutiwa moyo na wenzao wanahisi wataonekana wazaifu. Hapana  kwenye kila hali unaitaji kutiwa moyo ..

2.  Unatakiwa uanze kufanya  jambo

Kuanza ni kupiga hatua  ya uwajibikaji  calebu ndo wa kwanza kusema  "tukawaondoshe majitu" na ni calebu aliye mpa mpango   joshua nataka kwenda kuwaondoa wana wa anak katika mlima hebron. Huwez kuyashinda majalibu kama  usipo piga hatua ya kwanza.  Watu wengi wanashindwa kusonga mbele kwa sababu hawawez kupiga hatua .Hawataki kuwa waanzilishi wa jambo.

Ni kweli kuanzisha jambo kuna gharama lakini gharama zake  hazina maumivu ukisha fanikiwa.

 Waebrania 11:8

 Kwa imani Abrahamu alipoitwa aliitika, atoke aende mahali pale atakapopapata kuwa urithi; akatoka asijue aendako.

Ibrahimu aliambiwa na Mungu aache watu wake na kumfuata Mungu,  ni kweli ilimuuma lakini lengo la Mungu ni kumbariki Ilikuwa ngumu kwa mke wake Sarah's lakini kwasababu ibrahimu alikuwa ni different.  Alikubali......

Kutoka 3:3

Musa akasema, Nitageuka sasa niende nione kioja hiki, kwa nini kichaka hiki hakiteketei.

Moses aliona kichaka kinawaka moto akachukua hatua ya kukitazama  ndipo Bwana akaamua kuongea nae . Baada ya ile hatua Musa akawa mkombozi wa wana wa Israel. Ilikuwa ngumu kwake kwenda kuwakomboa lakini mkono Bwana ulikuwa juu yake.

 

Danieli 9:2

  katika mwaka wa kwanza wa kutawala kwake, mimi Danieli, kwa kuvisoma vitabu, nilifahamu hesabu ya miaka, ambayo neno la BWANA lilimjia Yeremia nabii, ya kuutimiza ukiwa wa Yerusalemu, yaani, miaka sabini.

Daniel alichukua hatua ya kusoma vitabu akajua miaka ya kuishi utumwani imeisha ,Mungu amekupa akili na maarifa ili uweze kufanya maamuzi  . Ukipiga hatua  ya kufanya jambo mungu atakupa  bonus .

3.  Unatakiwa kuwa na nia moja

Mithali 4 :25 Macho yako yatazame mbele, Na kope zako zitazame mbele yako sawasawa.

Kwenye kila jambo ambalo ni mapenzi ya Mungu, unatakiwa ku focus na kujitoa kwa moyo na akili ili ulifanikishe,  ndicho caleb ambacho  alikifanya  , tangu akiwa na 40 yrs  mpaka 80 yrs aliwaza kupata ile ahadi aliyo pewa na musa.

4.  Unatakiwa ufanye kazi kwa  moyo wako wote

Mfalme hezekia alisema kwenye neno lake alifanya kazi kwenye nyumba ya Bwana  alifanya kwa moyo wote  

2 wafalme 20:1-6 Siku hizo Hezekia akaugua, akawa katika hatari ya kufa. Isaya, nabii, mwana wa Amozi, akamjia akamwambia, Bwana asema hivi, Tengeza akasema,
Nakusihi, Bwana, ukumbuke sasa, jinsi nilivyokwenda mbele zako katika kweli na kwa moyo mkamilifu, na kutenda yaliyo mema machoni pako. Hezekia akalia sana sana.mambo ya nyumba yako; maana utakufa, wala hutapona.
Basi Hezekia akajigeuza, akaelekeza uso wake ukutani, akamwomba Bwana

Kalebu nae alifanya hivyo hivyo alitembea na Mungu kwa moyo wake wote

5. Unatakiwa uwe na uvumilivu

Kalebu alisubri mpaka ulipofika wakati sahihi wa Mungu , ndipo akamkumbusha Joshua  ahadi aliyopewa na mtumishi musa,

 Isaya 40 : 31  bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia

6. Usiache kukua  /kuongezeka

Mwanzo 1:28a

 Mungu akamwambia, Mimi ni Mungu Mwenyezi, uzidi ukaongezeke.

Katikati ya changamoto na  mlima unaoutaka  usiache kukua na kuongezeka .  jitahidi sana kuongezeka ki fikra, elimu na ki maendeleo kwasababu wakati ukifika wa kupanda kwenye mlima unatakiwa usikose, yamkini mlima wako ni biashara, basi kabla ujafungua hiyo biashara inabidi upate maarifa mengi kuhusu biashara,

 

 

Saturday, November 18, 2023

CHINI YA UONGOZI WAKE

‭‭2 Sam‬ ‭22:34‬ ‭
[34]  Huifanya miguu yangu kuwa kama ya kulungu; Na kunisimamisha mahali pangu pa juu.

Kuna faida kubwa sana kuwa under control na Mungu, kwasababu yeye ndo muumbaji na anajua mwisho na mwanzo wa maisha yako. Japo unaonekana ni mtu wa kawaida sana lakini jua Mungu anakutengeneza njia ya kufikia destiny yako.  

Ili uweze kufika destiny yako. Inabidi upite kwenye training tofauti tofauti  , na utakapo kuwa imara kwenye changamoto.  Mungu ataruhusu uingie kwenye pumziko ambapo ... 

Changamoto zikikufikia hauta tikisika, 
Endelea kukaa chini ya maongozo ya Mungu na ipo siku utafikia  kwemye top ya mlima unaopanda.

Yamkini mlima wako ni ndoa yako, masomo, kazi, uchumi, au mahusiano...  mpe awe kiongozi wako , ingia kwenye darasani lake, kubali maonyo yake.  Nawe utakuja kuwa  Daudi....

Monday, August 14, 2023

Nyenyekevu

 Luka chapter 5 verse 1 to 11

Biblia inatufundisha vitu 2

1. Unyenyekevu _petro

2. Nguvu ya Neno


Mungu hutumia watu wanyenyekevu ili kuwafanya wawe watumishi wake.

Petro aliombwa boti na Yesu ili awahubiri watu na akatoa . 

Petro hakumjua Yesu ni nani, petro hakumuwazia Yesu kama ni mtumishi wa uongo. Alimpa boti kwa moyo wake wote.


Watu wengi sasa huchagua watumishi na kudharau madhehebu.... Hawana unyenyekevu wala uvumilivu, wako tayari ku comment vibaya kazi Mungu kama wao walikuwepo kipindi Mungu anampa kazi mtumishi wake. 


Unyeyekevu ni njia mojawapo ambayo humfanya mtu kuwa na saburi, 

Unyeyekevu ni njia mojawapo ya kujilinda dhidi ya uadui.

Tujifunze kwa petro

Tuesday, June 27, 2023

Mtume Yohana (The revelator)

Watu wana mkubali sana apostle paulo  . Hata mimi namkubali. Ila kuna mwamba mmoja anaitwa apostle john The revelator.
Huyu mwamba  kipindi wanafunzi wa  Bwana Yesu wamemkimbia Yesu Kristo.  Yeye alibaki  na kusema kama kufa nitakufa nae. Hakutoka pale chini ya msalaba till End.

Ndiye mwanafunzi wa Yesu ambaye kifo chake hakikuwa cha kikatili, 
Injili alizoandika zote zilikuwa zakuonyesha Upendo wa Yesu.  
He is the Lover Man
Alikuwa ndo mtume mdogo kuliko wote. 
Na ndiye aliishi miaka mingi.....

Mitume wangekuwa katika watoto wa Yakobo basi ningemfananisha na Benjamin 
Maana alikuwa madogo kuliko wote na alipata vitu vingi katika mgao wa zawadi za Yusuph.Alikuwa kipofu lakini aliona yaliyo sirini...
Aliandika akasema Yesu ndiye Alpha & omega

Friday, December 30, 2022

KUENENDA KWA HEKIMA NDANI NA NJE YA WAAMINI

Enendeni kwa hekima mbele yao walio nje, mkiukomboa wakati. Maneno yenu yawe na neema siku zote, yakikolea munyu, mpate kujua jinsi iwapasavyo kumjibu kila mtu.
Kol 4:5‭-‬6 

Mtume paulo anatukumbusha kuhusu kuishi kwa jinsi gani sisi tulio katika imani Yetu.
Mtume paulo anasema kuwa tuenende kwa hekima . Lakini mbele anaongezea kuwa mbele yao walio nje. 
Hekima ni nini. 
Ni maisha ya kuishi kwa busara na unyenyekevu na kuto vunja sheria unaopelekea kumpendeza jirani yako na Mungu pia. 
Hekima hupelekea amani, 
Hekima huleta furaha
Mtume paulo aliposema tuenende kwa hekima alitaka tuwe watu wanaopeleka amani sehemu . 
Kwaiyo sisi tuliokoka tunaitaji sana tuwe na hekima ili jina la Yesu lisitukanwe. Na pia tunaenenda kwa hekima mbele za watu tutawavuta watu waje kwa Yesu
Naweza sema kuwa tunapo enenda kwa hekima tunakuwa tunafanya uinjilishaji . 

Kwa sababu pale tunaoonyesha matendo yetu mema watatamani wajue sisi ni wakina nani na tumetokea wapi. Wakijua tutakuwa tumemuinua Yesu juu. 

Maisha ya Yesu Kristo yalikuwa ni ya hekima. Tuone maisha yake
1. Alikaa na wenye zambi
2. Aliponya na hakutaka kujulikana
3. Aliunganisha jamii na jamii (mwanamke msamaria)
4. Alikubali kusikiliza watu. (Mwanamke na makombo)
5. Alifundisha kwa mifano
Hii ni mifano ya Yesu alipotembea kwa hekima.

PART 2. Continue.....

Friday, December 16, 2022

Nani aliye mlangoni mwa Moyo wako?

Hata wakati wa chakula cha jioni; naye Ibilisi amekwisha kumtia Yuda, mwana wa Simoni Iskariote, moyo wa kumsaliti;
Yn 13:2 

Biblia inaambia kuwa Yuda alikwisha wekewa roho ya usaliti.  Kwaiyo usaliti hauji tu kwa mtu kupenda ila ni kazi ya shetani.  Na hii inatokana na kumwachia shetani mlango wa moyo wako.
Tunaitaji sana kuliweka neno la kristo katika moyo wetu ili mharibu ajapo jalibu kuingiza chuki ndani ya moyo wetu akute kumejaa Neno la uzima.  

Yesu alikuja duniani ili tuwe na uzima tele. Uzima tele alikuwa na maana katika kila kitu ufanikiwe na kuonekane wema wa Mungu . Moyo wa mwanadamu umeumbiwa amani kufurahi na kupokea yaliyo mema kutoa yaliyo mema.  

Kwaiyo unapo mpokea Yesu kuwa Bwana na mokozi wa maisha yako anakuletea uzima ndani ya moyo wako. Ndo maana watu wengi wanaojazwa Neno la uzima katika mioyo yao wanakuwa na amani siku zote.

Tafuta watu wanaoenda kanisani na mizigo ya maisha . Wakitoka tu kanisani wanakuwa ni wepesi kwa sababu ya Nenola uzima wanalopokea kwa makuhani wao.

Kwaiyo tunaitaji sana kumkimbilia Yesu kristo ili shetani asituingizie roho za giza. Kwa maana kama aliweza kumdanganya eva anaweza kukudanganya na wewe  kama aliweza kumdanganya yuda anaweza kukudanganya nawewe. 

Nakuombea kwa Jina la Yesu kristo wa Nazareth  Roho mtakatifu akulinde na azidi kukuongoza katika njia ya imaniili shetani asiwe mdanganyifu 
AMEN.

Friday, June 17, 2022

UTUKUFU WAKE YESU

Lakini, kueni katika neema, na katika kumjua Bwana wetu na Mwokozi Yesu Kristo. Utukufu una yeye sasa na hata milele.
2 Pet 3:18 

Tukue  na Tufanikiwe kwenye
 1. Ndani ya Neema
2. Katikati ya kujifunza kumjua Mungu

Kwanini tukue na tufanikiwe

Kwa sababu  Yesu anao utukufu 

Kama tukiongezeka na kufanikiwa basi tutapata utukufu wake.

Utukufu maana yake ni uwepo wa Mungu katikati ya maisha yako.

Amen

Tuesday, December 28, 2021

MUUNGANIKO WA KIROHO KATI YA MAMA NA KIJANA...

 

Yh 19:26 -27

Basi Yesu alipomwona mama yake, na yule mwanafunzi aliyempenda amesimama karibu, alimwambia mama yake, Mama, tazama, mwanao.

 Kisha akamwambia yule mwanafunzi, Tazama, mama yako.

 Na tangu saa ile mwanafunzi yule akamchukua nyumbani kwake.

 Mifano ya kwenye biblia_ 

- Yesu na mama yake
-Yabesi na mama yake
- samweli na mama yake
- Sarah na isaka



1 wafalme 4 : 10
Tukimsoma Yabesi alipewa jina kutokana na   hali ya uzuni iliyotokea kwa  mama ake . Ndipo akampa jina lake Yabesi

- Hapa tunakumbushwa kuna connection ya kiroho katika ya mama na mwana ambayo ilimhathiri mtoto

2. Pia tukimsoma  hannah jinsi ya kumpata samweli  tunaona kuwa  hakumpata kwa jinsi ya kawaida bali alikaa vizuri kiroho na Bwana akampatia Mtoto ambaye alikuwa nabii.....

3. Kuhusu isaka na sarah tunaona kuwa  Tumbo la wana wa Mungu huzaa wafalme..... kwaiyo Tunaitaji sana  kuwaombea binti zetu  ili Mungu aweze Kuweka wafalme ndani yao.

Tujifunze 

.Mzazi /Mama kuwaombea vijana wao mpaka kusudi la Mungu lijengeke ndani yao 

.Kuna baraka unapowakumbuka wazazi 

.Mungu hutumia wazazi kuwa baraka. Haijalishi kazeeka , au hajaokoka lakini kwa kuwa alikutunza still bado kuna connection ya rohoni.

Saturday, December 18, 2021

Mshukuru Mungu

Kuna aina nyingi za kumshukuru za Mungu 

1. Kabla ya kukupa kitu
2. Baada ya kukupa kitu
3. Umepata au hujapata
4. Umekosa vyote... 

1.    unaweza kupitia magumu kama ayubu . Mshukuru Mungu 

akasema, Mimi nilitoka tumboni mwa mama yangu nili uchi, nami nitarudi tena huko uchi vilevile; BWANA alitoa, na BWANA ametwaa; jina la BWANA na libarikiwe.
Ayubu 1:21 

2.umepata kitu kwa uchache . Mshukuru Mungu 

Basi Yesu akaitwaa ile mikate, akashukuru, akawagawia walioketi; na kadhalika katika wale samaki kwa kadiri walivyotaka.
Yohana 6:11 

3. Umeponywa kama wakoma kumi , rudi kumshukuru mungu 

akaanguka kifudifudi miguuni pake, akamshukuru; naye alikuwa Msamaria.
Luka 17:16 

4  . Umepata / haujapata mshukuru Mungu maana bado anakufadhili .......

Haleluya. Mshukuruni BWANA kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Zab 118:1 

Kuna nguvu katika kumshukuru 💪💪

Tuesday, November 16, 2021

MAOMBI YAKO YALIYOCHELEWA KUJIBIWA


Daniel 10:13 

Lakini mkuu wa ufalme wa Uajemi alinipinga siku ishirini na moja; bali, tazama, huyo Mikaeli, mmoja wa hao wakuu wa mbele, akaja kunisaidia; nami nikamwacha huko pamoja na wafalme wa Uajemi.

Katika mistari hii tunapata kuona kazi za malaika 

Kwa uelewa wangu wapo malaika wa aina nyingi baadhi ninao wajua ni
1. Malaika wa vita
2. Malaika wapeleka ujumbe wa amani
N.k

Hapa tunaona malaika wa vita na malaika mpeleka ujumbe wa amani. Ambao pia tunawaona kwa mariamu magdalena (luka 1 :26_45) na kitabu cha yuda ( yuda 1:9)

Katika kitabu cha Daniel. Tunaona malaika alikuja kuleta majibu ya maombi Daniel lakini katika ulimwengu wa kiroho ufalme wa uajemi walizuia maombi hayo .

Hapa tunapata kitu kwamba kuna vitu . Kuna aina ya maombi ambayo tunatakiwa kujifunza ili kuharibu mipango ya wafalme wa anga ambao wanazuia maombi yetu yasijibiwe.

Daniel alikuwa ameokoka lakini maombi yake yalizuiliwa.

Lakini kuna maombi ambayo tunaweza kuomba mbingu zikafunguka na kupata majibu 

Yamkini ugonjwa, kupata kazi, kupata amani, uchumi wako kukua.

Kuna funguo za kupata majibu yako . Kama

Tafuta vifungu vya biblia vinavyo husika na ufunguo.. 
Mfano ufunuo 3 :7

Thursday, November 11, 2021

HIYO KWELI ITAWAWEKA HURU

Basi Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini,

 Ninyi mkikaa katika neno langu, mmekuwa wanafunzi wangu kweli kweli; tena mtaifahamu kweli,

 nayo hiyo kweli itawaweka huru.

Yn 8:31‭-‬32 SUV



Neno la Mungu  ni Lihai na ni pumzi ya Mungu  

hii inatufanya kujenga hoja kwamba Neno la Mungu ni roho ya Mungu kutokana na isaya 11 : 2

Na roho ya BWANA atakaa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, roho ya maarifa na ya kumcha BWANA;

Hivyo basi kwa kadri unavyokaa ndani ya maneno ya Mungu , automatically  nafsi yako inajiconect na Neno la Mungu (roho saba za Mungu)

Hivyo basi unajikuta unapata ufahamu  ndani ya maisha Yako kwenye kila tatizo linalokusibu

Pia kama kuna vitu vilikuwa haviendi kwenye maisha yako unakuta vinaenda kwa sababu Neno la Mungu linakuwa linajiendesha ndani ya akili yako, mwili wako, roho yako, 

Neno la Mungu ni kama mfumo/mashine ambayo imeingia ndani ya Maisha yako ambayo inatatua matatizo kwa urahisi.

Unapofanya maombi ukisema imeandikwa... pale una active mashine nafsini mwako ambayo hiyo mashine ni Neno la Mungu. Unakuta maombi yako yanapata majibu na hapo ndipo Yesu anasema NA HIYO KWELI ITAKUWEKA HURU. 

ni maombi yangu majibu ya maombi yako yajibiwe kwa jina La Yesu kristo

Tuesday, October 5, 2021

MUNGU YUPO NA ANAKUSIKILIZA MAOMBI YAKO.

Isaya 41:21

Haya, leteni maneno yenu, asema Bwana; toeni hoja zenu zenye nguvu, asema mfalme wa Yakobo.

Mungu anatupa nafasi sisi watoto wake tuweze kuongea kile kitu ambacho tunataka tufanye, tufanyiwe, kitokee au kisitokee.

 

Hoja zenye nguvu

Mungu anatupa ruhusa ya kujadiliana naye mambo yetu ambayo tunataka kumshilikisha.

Mungu anataka tutumie akili na moyo pale tunapo taka kusema naye,

Tunapoenda mbele za Mungu tutumie moyo ili tuweze kuweka Imani zetu kwa yeye ili tupate itaji letu.

Imani juu ya unacho kiomba basi utapokea.  

Ebrania 10 : 38

Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita, roho yangu haina furaha naye.

Imani inakaa mioyoni [ warumi 10 : 10 Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu ]

 Isaya 1:18a

Haya, njoni, tusemezane, asema Bwana. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu.

Kwenye biblia ya kingereza kasema come now let us settle the matter

Settle : to reach a decision or an agreement about something, or to end a disagreement:

Hapa bado Mungu anatusogeza  karibu, kwa njia ya kusolve tatizo , yaani kuyajenga, kuondoa tofauti zetu.

Mungu wetu alituumba akatupa uhuru wa kufanya jambo,

Tuko  tofauti na viumbe vingine, Ametupa nafasi sisi wanadamu wa kujielezea mbele zake na hii ndio maana ya upendo (uhuru)

Mathayo 7 :7

Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa;
8 kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa.
Au kuna mtu yupi kwenu, ambaye, mwanawe akimwomba mkate, atampa jiwe?
10 Au akiomba samaki, atampa nyoka?

Bado mungu anaonyesha ukaribu na wanadamu yakuwa  chochote tutapata ila tumuombe yeye.

Kuna vitu vitatu katika mstali huu

1.     Omba ( ask)

to put a question to someone, or to request an answer from someone

2.     Bisha  ( knock)

to repeatedly hit something, producing a noise:

3.     Tafuta  ( seek )

to try to find or get something, especially something that is not a physical object:


Tunao uwezo wa kumshawishi Mungu tukiwa na Hoja zenye nguvu.

 Mathayo 11:12

Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka.

Kjv bible

12And from the days of John the Baptist until now the kingdom of heaven suffereth violence, and the violent take it by force.

Suffereth  means  with unwilling permission

Violent means using force to hurt or attack

Biblia inasema ufalme wa mbinguni unapatikana kwa nguvu nao wenye nguvu wauteka

Anaposema ufalme wa mbinguni anamaanisha;-

1.     Vitu  vizuri vya mbinguni

2.     Mamlaka ya kutawala ya mbinguni

3.     Uhuru ambao uko mbinguni

4.     Amani iliyokuwa mbinguni

Kuupata kwa nguvu anamaanisha kuufanyika kazi mpaka upate,

Kuuteka

-      Anaposema kuuteka Anamaana hatupewi, ila tunachukua bila lidhaa, yaani hatukustahili kuwanacho ila tunakuwa nacho.

-      Hukustahili kupata kitu flani ila unakipata.

Nakuombea ifike level ambayo kuna kazi ulitakiwa kuikosa, kwakuwa unazo nguvu za rohoro uipate kwa jina la Yesu ”.

 

Mifano ya watu ambao walikuwa na hoja na nguvu ambazo zilibadili mambo yao.

 

Ibrahimu                 (Mwanzo 18:19-30

19 Kwa maana nimemjua ya kwamba atawaamuru wanawe, na nyumba yake baada yake waishike njia ya Bwana, wafanye haki na hukumu, ili kwamba Bwana naye akamtimizie Ibrahimu ahadi zake.
20 Bwana akasema, Kwa kuwa kilio cha Sodoma na Gomora kimezidi, na dhambi zao zimeongezeka sana,
21 basi, nitashuka sasa nione kama wanayotenda ni kiasi cha kilio kilichonijia; na kama sivyo, nitajua.
22 Basi wale watu wakatoka huko wakaelekea Sodoma; lakini Ibrahimu alikuwa akali akisimama mbele za Bwana.
23 Ibrahimu akakaribia, akasema, Je! Utaharibu mwenye haki pamoja na mwovu?
24 Huenda wakawapo wenye haki hamsini katika mji, utaharibu, wala hutauacha mji kwa ajili ya hao hamsini wenye haki waliomo?
25 Hasha usifanye hivyo, ukamwue mwenye haki pamoja na mwovu, mwenye haki awe kama mwovu. Hasha; Mhukumu ulimwengu wote asitende haki?
26 Bwana akasema, Nikiona katika Sodoma wenye haki hamsini mjini, nitapaacha mahali pote kwa ajili yao.
27 Ibrahimu akajibu, akasema, Basi, nimeshika kusema na Bwana, nami ni mavumbi na majivu tu.
28 Huenda wakapunguka watano katika wale hamsini wenye haki, je! Utaharibu mji wote kwa kupungua watano? Akasema, Sitauharibu, nikiona humo arobaini na watano.
29 Akazidi tena kusema naye, akinena, Huenda wakaonekana humo arobaini? Akasema, Sitafanya kwa ajili ya hao arobaini.
30 Akasema, Bwana asiwe na hasira, nami nitasema, Huenda wakaonekana huko thelathini? Akasema, Sitafanya, nikiona humo thelathini.

 

Musa                     (Kutoka 32:9-14

Tena Bwana akamwambia Musa, Mimi nimewaona watu hawa, na tazama, ni watu wenye shingo ngumu
10 basi sasa niache, ili hasira zangu ziwake juu yao, niwaangamize, nami nitakufanya wewe uwe taifa kuu.
11 Musa akamsihi sana Bwana, Mungu wake, na kusema, Bwana, kwa nini hasira zako kuwaka juu ya watu wako uliowaleta kutoka nchi ya Misri kwa uweza mkuu, na kwa mkono wenye nguvu?
12 Kwa nini Wamisri kunena, wakisema, Amewatoa kwa kuwatenda uovu, ili apate kuwaua milimani, na kuwaondoa watoke juu ya uso wa nchi? Geuka katika hasira yako kali, ughairi uovu huu ulio nao juu ya watu wako.
13 Mkumbuke Ibrahimu, na Isaka, na Israeli, watumishi wako, ambao uliwaapia kwa nafsi yako, na kuwaambia, Nitazidisha kizazi chenu mfano wa nyota za mbinguni; tena nchi hii yote niliyoinena nitakipa kizazi chenu nao watairithi milele.
14 Na Bwana akaughairi ule uovu aliosema ya kwamba atawatenda watu wake.

 

 

 

Mfalme Hezekia           (Isaya 38:2-6)

Basi Hezekia akajigeuza, akaelekeza uso wake ukutani, akamwomba Bwana,
akasema, Ee Bwana, kumbuka haya, nakusihi, kwamba nimekwenda mbele zako katika kweli na kwa moyo mkamilifu, na kutenda yaliyo mema machoni pako. Hezekia akalia sana sana.
Ikawa, neno la Bwana likamjia Isaya, kusema,
Enenda ukamwambie Hezekia, Bwana, Mungu wa Daudi, baba yako, asema hivi, Mimi nimeyasikia maombi yako, nimeyaona machozi yako; tazama, nitaziongeza siku zako, kiasi cha miaka kumi na mitano.
Nami nitakuokoa wewe, na mji huu, na mkono wa mfalme wa Ashuru, nami nitaulinda mji huu.

 

Hannah                  (1 Samweli 1:14-20)

14 Ndipo Eli akamwambia, Je! Utakuwa mlevi hata lini? Achilia mbali divai yako.
15 Hana akajibu, akasema, Hasha! Bwana wangu, mimi ni mwanamke mwenye roho ya huzuni, mimi sikunywa divai wala kileo, ila nimeimimina roho yangu mbele za Bwana.
16 Usimdhanie mjakazi wako kuwa ni mwanamke asiyefaa kitu; kwa kuwa katika wingi wa kuugua kwangu na kusikitika kwangu ndivyo nilivyonena hata sasa.
17 Ndipo Eli akajibu, akasema, Enenda kwa amani; na Mungu wa Israeli akujalie haja yako uliyomwomba.
18 Naye akasema, Mjakazi wako na aone kibali machoni pako. Basi huyo mwanamke akaenda zake, naye akala chakula, wala uso wake haukukunjamana tena.
19 Wakaondoka asubuhi na mapema, wakasali mbele za Bwana, kisha wakarejea na kufika nyumbani kwao huko Rama; Elkana akamjua mkewe Hana; naye Bwana akamkumbuka.
20 Ikawa, wakati ulipowadia, Hana akachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; akamwita jina lake Samweli, akisema, Kwa kuwa nimemwomba kwa Bwana.

 

 

Yabesi                     (1 Nyakati 4:9:10)

Naye Yabesi alikuwa mwenye heshima kuliko nduguze; na mamaye akamwita jina lake Yabesi, akisema, Ni kwa sababu nalimzaa kwa huzuni.
10 Huyo Yabesi akamlingana Mungu wa Israeli, akisema, Lau kwamba ungenibarikia kweli kweli, na kunizidishia hozi yangu, na mkono wako ungekuwa pamoja nami, nawe ungenilinda na uovu, ili usiwe kwa huzuni yangu! Naye Mungu akamjalia hayo aliyoyaomba.

Nakuombea yakuwa Mungu azidi kukufungulia Neema ya kuisikia sauti yake. AMEN

Saturday, March 27, 2021

Yesu kiongozi Mwema

Na tazama, wakamletea mtu mwenye kupooza, amelala kitandani; naye Yesu, alipoiona imani yao, alimwambia yule mwenye kupooza, Jipe moyo mkuu, mwanangu, umesamehewa dhambi zako. Na tazama, baadhi ya waandishi wakasema nafsini mwao, Huyu anakufuru. Naye Yesu, hali akijua mawazo yao, akasema, Mbona mnawaza maovu mioyoni mwenu? Kwa maana rahisi ni lipi, ni kusema, Umesamehewa dhambi zako, au ni kusema, Ondoka, uende? Lakini mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi, (amwambia yule mwenye kupooza) Ondoka, ujitwike kitanda chako, uende nyumbani kwako.
Mt 9:2‭-‬6 SUV

Kiongozi wetu Yesu kristo anatufundisha vitu katika sura hii jinsi alivyo kutana na changamoto au jina lingine niite jinsi ya alivyokutana na  fursa ya kumponya mwenye kupooza

Kuna vitu vinne ambavyo anatufundisha katika mistari hii.

1. Huruma
Tunaona Yesu kristo kama Mungu mwanadamu aliyekuwa na uwezo na mamlaka ya kufanya chochote hapa duniani alikuwa na huruma kwa wanadamu ,  kama alivyo mwambia Yule mwenye kupooza 
Jipe moyo mkuu mwanangu, umesamehewa zambi zako
Tukisoma hayo maneno aliyosema Yesu tunakuta anatufundisha kuwa tunatakiwa tuwe na moyo wa huruma wakusaidia watu kwa njia yoyote.  Awe mwamini au sio mwamini kwa sababu ni moja ya jambo jema kwa Bwana.

2. Mamlaka
Wakristo wwngi sana huwa tunaogopa kutamka vitu vya mungu vilivyo moyoni kwakuwa tunaogopa kama watu watatusema vibaya na kutuona tuna makosa. Lakini tunasahau ya kuwa tumepewa mamlaka  na funguo Juu mbinguni na Duniani,  kwa kila jambo jema lenye kumpendeza Mungu  kwa sababu kwa kila mambo safi Roho mtakatifu hufanya kazi na hao wafanyayo hayo.
Lakini paulo mtume wa Yesu anatukumbusha kuwa tunatenda kazi kwa kadri ya nguvu ifanyayo kazi ndani yetu. Kwaiyo hatutakiwi kuogopa  kufanya jambo jema ambalo mamlaka ya mbinguni inakubaliana na sisi,  Yesu alikuwa na mamlaka ya kumponya na kumsamehe yule aliye pooza kwa kiwa lilikuwa ni jambo jema.

3. Uweza
Watu wengi tuna changamoto ya kubadili tafsiri ya mambo ya rohoni kuwa katika mwilini (physical)  
Yesu alikuwa na uwezo wa kutamka kilicho rohoni kwake kikawa katika hali ya mwilini,  

Je kwanini vitu vya rohoni havitokei kwa jinsi ya mwilini?

a. Hatuombi sawasawa na mapenzi ya Mungu
b. Hatuna mbegu ya imani.

Hizi ni baadhi ya vitu ambavyo vinafanya vitu vya rohoni kuonekana katika ulimwengu halisia . 

4.kutia moyo au kusaidia huduma au kazi za watu wengine.

Yesu kristo kiongozi wa imani yetu 
Aliona imani na juhudi ya wale watu ambao walimbeba ndugu mwenye kupooza.
Hivyo akafanya huduma ya kumponya yule mtu,  na tunaona watu wengi wanashindwa kuona juhudi  za watu wengine  na hata kuwatia moyo , hata pengine  kuwapa neno la hekima ili wasonge mbele katika familia zao, 
Lakini pia hata kuomba pamoja nao, katika hali wanayo pitia,  maana tunaona hata Yesu  aliwachukua baadhi ya wanafunzi kwenda kuomba nao mlimani, na hii inatufundisha kuwa alitaka wamtie moyo katika hali zote za huduma yake,

Lakini hata alipofunga siku 40, tunaona kuwa malaika walikuwa pamoja nae wakimhudumia, 
Lakini pia hata musa na eliya walishuka kumtia moyo...

Mwisho Yesu kabla ajampa uponyaji huyu mtu mwenye kupooza alianza kwa kumwambia habari njema . Umesamehewa dhambi zako.  hivyo basi katika huduma yoyote tunatakiwa tuna waambia watu habari njema za Mungu.



Wednesday, March 24, 2021

MAOMBI YASIO YA UBINAFSI

Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii.
Yak  ‬15‭-‬16 

Biblia inatufundisha vitu 3
1. Toba
2. Maombi
3.bidii

Toba
Tunafundishwa kuwa tukumbuke kuomba toba kwa ajili ya yetu na wenzetu,
Watu wengi wakienda mbele za Mungu hawakumbuki kuomba toba kwa ajili ya wengine..... ,  na hii hupelekea maombi yao kutojaa majibu yanayostahili katika kuomba kwao. 

Tunaomba toba si kwamba tumetoka kufanya dhambi ,hapana bali unapoenda mbele za Mungu  lazima ujitakase kwa maana yeye ametukuka, pia sisi sio wakamilifu kwaiyo tunaitaji damu ya Yesu ili tuweze kufika katika ukamilifu wa Mungu. 

2. Maombi

Watu wengi tunapoenda kuomba huwa tunaenda kwa ajili ya maendeleo yetu na sio maendeleo ya wenzetu .

 Tunaona kuwa Yesu alituombea sana kuliko kujiombea yeye, hapa anatufundisha kuwa mpende jirani yako kama nafsi yako,  na hii ndio huduma ambayo Mungu anataka , maana alisema anatafuta mtu katika nchi ili alijenge boma, yaani sehemu iliyobomoka , kubomoka wapi sio kwake huyo mtu bali taifa,kanisa ,familia ,jamii .... 

3. Bidii

Lakini tunaona kuwa biblia inatufundisha kuwa kuomba kwa mwenye haki kwafaa kuomba kwa bidii, kwaiyo tunatakiwa tuwe watu wa kuomba sana na kwa ufasaha, 
To be continue......

Friday, November 20, 2020

UNAONA NINI JUU YA WATOTO WAKO

.

Uwe hodari na moyo wa ushujaa, maana ni wewe utakayewarithisha watu hawa nchi hii niliyowaapia baba zao ya kwamba nitawapa.

Kuna watoto ambao wamezaliwa kwa ajili ya kufanya kusudi la Mungu , wengine wanatimiza maono ya babu zao, au wazazi wao. 

Wengine wana malizia huduma iliyo anzishwa na ndugu zao, na wengine wanaweka msingi wa huduma kwa ajili ya kizazi chake kitakacho kuja,  
Anaweza asiwe mtoto wako wa kumzaa lakini anapenda kile kitu ulicho nacho, kama wewe mhubiri na yeye anatamani kuwa ni mhubiri, kama mwimbaji anaweza kutamani kuwa mwimbaji, hawa wote tunaita ni watoto, 

GAL. 4:19‭-‬20 SUV
Vitoto vyangu, ambao kwamba nawaonea utungu tena mpaka Kristo aumbike ndani yenu; laiti ningekuwapo pamoja nanyi sasa, na kuigeuza sauti yangu! Maana naona shaka kwa ajili yenu.

Paulo anatujulisha kuwa alikuwa na watoto ambao alikuwa anawashape ili kazi alioanza isiwe bure iwe kizazi hata kizazi, kwaiyo kazi ya Mungu haina hasara Mungu akikupa nafasi ya kuishi nyakati tofauti tofauti anakupa watoto ambao watabeba kilicho chako ili utakapo maliza safari yako , wawepo wengine wakuendeleza gurudumu. 

EZE. 22:30 SUV
Nami nikatafuta mtu miongoni mwao, atakayelitengeneza boma, na kusimama mbele zangu mahali palipobomoka, kwa ajili ya nchi, nisije nikaiharibu, lakini sikuona mtu. 

Kuna watu ambao hawajawahi waza kama nikifa au nikimaliza kazi, je nitamwachia nani? Hapa inaonekana katika hiyo nchi hakukuwa na mtumishi hata mmoja. Au walikuwepo wakafa na vitu vyao, hawakurisisha huduma kwa kizazi kingine... 

Lakini pia

Mungu anatukumbusha kwenye mstari huu kuwa anatafuta mtu miongoni mwa watu ili aweze kusimama mbele zake na kuchukua  vya kwake vidhihirishwe duniani.   Unaweza ukasema kuwa nyumba yangu yoote wameokoka , au ukoo wangu woote wameokoka lakini hayupo hata mmoja ambae amebeba kazi ya Mungu. 

Wapo wazazi ambao wanajua kuwa mtoto wake anakitu lakini anapuuzia . Kile kitu kitakuwepo lakini shetani akija anakiiba unakuta mtoto alianza vizuri kuimba kanisani baadae unakuta anaimba mapenzi, alikuwa mhubiri mzuri anakuwa MC unakuja alikuwa anakipawa cha kuomba unakuta anapenda kukaa sana kijiweni...

Inapelekea baadae kile kitu kinapoa, Mungu anasubiri miaka 25 baadae yule mtoto kakuwa naye anawatoto Mungu analudisha kipawa kwa mtoto wake ..... 

NINAKUOMBEA KWA JINA LA YESU KRISTO  

Uwe productive katika huduma uliyopewa

Ujue kilicho ndani ya watoto wako na wajukuu wako

Mungu aseme na wewe kuhusu kurisisha huduma kwa wengine

Ukumbe kuwaombea na ufalme wa Mungu ukae ndani ya watoto wako

Kile  ulichowapa watoto wako ukiombee mpaka kitakapo timia kwa wakati wake.

Part 2

Itaendelea......

See 👉  Yoshua 1 :6

Tuesday, October 13, 2020

HOFU YA MUNGU

Akaingia nyumbani kwake akasema, Salamu, uliyepewa neema, Bwana yu pamoja nawe.

 Naye akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake, akawaza moyoni, Salamu hii ni ya namna gani?

 Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu.
Luka 1 : 28 _30

Shalom, 

Biblia inasema Naye akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake, akawaza moyoni...

Kuna wakati ukienda mbele za Mungu unajikuta kuwa na hofu sana.

Na kuna wakati hata kama ujaenda mbele za Mungu unajihisi hofu mpaka unajikuta unaomba toba. Ukiona hali hiyo jua kuwa....

Utukufu wa Mungu umekuzukia na Roho mtakatifu anataka kusema na wewe, anataka kukupasha habari....

Tuesday, September 29, 2020

ROHO YA MATENGANO

Basi ndugu, nawasihi, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba nyote mnene mamoja; wala pasiwe kwenu faraka, bali mhitimu katika nia moja na shauri moja.

1 KOR. 1:10 

Mtume paulo anatukumbusha kuwa  katika maisha ya kila siku tujitahidi sana tuwe tunaongea lugha moja au jina lingine tuongee vitu vyenye maana moja, ili kati yetu kusiwe na mgawanyiko.   

Hii tumeiona baada ya watu walipogaqanyika wengine wa paulo na wengine apollo.

That means apollo alikuwa na aina yake ya kufundisha na paulo pia. Kwaiyo watu wakajikuta wanatafuta ubora . Ambacho hicho kitu hakitakiwi  kabisa katika huduma ya Mungu, 

2. Pia mafarakano mengi yanatokea pale ambapo watu walio elimika wanataka kusikilizwa  na kupuuzia mawazo ya wengine

Nikwambie kitu , biblia inasema kuwa tufanye kazi ya Mungu kwa hekima yote, ana maana kuwa tujitahidi sana kutumia hekima ili Neno la Mungu lipokelewe kwa furaha.

3. Kutumia hekima ya kukaa kimya.

Biblia inatufundisha  ni heri kuwa msikilizaji utaonekana kuwa una hekima kuliko kuwa miongeaji. Lakini pia hii inatukumbusha wakati wa esta na naamani, esta alipo sikia yale mambo alikaa kinya na kufunga kwa siku tatu ili apate kibali kwa Mungu na kwa mfalme, ili aliseme jambo lake. Lakini tunaona kuwa alifanikiwa ,  biblia inasema kuna wakati wa kusema na wakati wa kunyamaza. So ukiona kuna mtafaluku katika kundi au kanisa au familia kaa kimya kwa muda tafuta hekima ya Bwana ,ili usubiri hekima ya kimungu ije juu yako.

4. Kutii 

Biblia inatuhimiza kuwa tutii amri iliyo kuu. Maana zote zinatoka kwa Bwana.  Endapo katika uongozi wa kitaifa, nyumba au kanisa au jamii. Kama kuna wazo hujapendezwa nalo basi kutii ni bora kuliko mafuta ya beberu. Maana Bwana anajua na  anasababu,  tunakumbuka stori ya nebukadreza alivyoambiwa na Bwana kupitia maneno ya mtumishi wake danieli kuwa aweke sawa ufalme wake kabla ya kuharibiwa. Alipuuzia na akaishi misimu mingi kama mnyama. Lakini baadae aliludi kwenye uongozi na kuandika Mungu wa danieli ni Mungu wa kweli. 

Ili tusiweze kufarakana ni bora tuwe tuna tii, maana Bwana anataka tuwe wana maombi , tumuulize yeye kwanini hili linatokea, naye atatupa kujua na1 kurekebisha . 

Ni maombi yangu kwa ajili yako.

Bwana akupe moyo na tunda la uvumilivu, 

Bwana Akupe tunda la kupokea mafundisho ya watumishi mengine

Bwana akupe roho ya hekima 

Bwana akupe roho ya umoja

Bwana aondoe roho ya matengano

Amen...

Friday, May 1, 2020

MCHUNGAJI MWEMA

Wakati kama huu ni wakati wa kung'ang'ana na Yesu na kulisoma Neno lake ili tuweze kusikia atakoacho tuambia, shetani akileta sauti ya  hofu atuwezi kuisikia maana masikio Yetu yapo kusikia sauti ya mchungaji mwema Yesu... 

Kwaiyo wale wampendao watajitahidi sana kusoma Neno lake na kufanya maombi kwa kwa jinsi ya mapenzi yake. 

Lakini pia watatamani malisho yake yaani Neno lake lisiwapite wakati wote na Muda wote... kama jinsi unavyokula chakula cha asubuhi, mchana na jioni..

Mwili unaitaji chakula ili uweze kutengeneza nguvu mwilini , lakini pia roho inaitaji chakula kama mwili  ili iweze kusimama katika imani, 
Kwaiyo tukiwa na Yesu na akitupa chakula chake kila siku, imani Yetu inajengeka na tutakuwa imara siku hadi siku, tutapanda imani hata imani, utukufu hadi utukufu. 

Katika nyakati zote  za njaa, ziki, utumwa, hata za magonjwa tusome Neno la Mungu ...

See 👉 Yohana 10 : 4.

#covid19, #Goodnews,

Monday, April 13, 2020

NEEMA ULIOPEWA SI BURE

Kupata zawadi/Neema ya kuokoka si mwisho, mpaka ukarizika. Hapana Fanya jambo kwa Yesu, zaa matunda , weka jambo katika dunia.

 Ili hiyo Neema uliopewa  isiwe ya Bure, kumbuka  mavuno ni mengi ,watenda kazi wachache
👉 1wakoritho 15: 10

YESU WA WATU WOTE

Kuna mambo ambayo Yesu anakufanyia katika maisha yako kwa mfano  uponyaji, mafanikio, amani ,msamaha, ukombozi,

Kwa nini ?

 ili watu walio kalibu na wewe,  wajue  jinsi gani Yesu alivyo mzuri, na ili walio na dhambi wakumbuke yuko Mungu  ambaye  anawapenda na anaweza kuwaokoa na kuwasamehe.
👉  marko 5 : 19 - 20

Thursday, March 19, 2020

YESU BADO ANATUPENDA

Mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwengu; bali uwalinde na yule mwovu. Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndiyo kweli. Yohana 17 : 15

TUZIDI KUSOMA NENO LA MUNGU, YESU ALISHATUOMBEA KWA MUNGU BABA KWAMBA MUNGU ATATULINDA DHINI YA MASHAMBULIO YA MWOVU SHETANI.

HAIJALISHI UGONGWA ULIOTOKEA CHINI YA BAHARI (CORONA VIRUS)  AU ARDHINI, AU JUU YA ANGA..  

 MAADAMU UNAMPENDA YESU NA UNALISOMA NENO LAKE. UNAO UJASIRI WA KWENDA KWAKE KUOMBA LOLOTE.  

KAMA WANA WA ISRAELI WALIVYO WEKA DAMU YA KONDOO  KATIKA  MILANGO YAO KULE MISRI ,
NDIVYO CHAPA YA YESU ILIVYO NDANI YA MIOYO YETU TUNAPO SOMA NENO LAKE. 
 

Saturday, December 7, 2019

BARAKA ZA KIUONGOZI



 Kila mahali zitakapopakanyaga nyayo za miguu yenu, nimewapa ninyi, kama nilivyomwapia Musa. 

Tangu jangwa hili na mlima huu, Lebanoni, mpaka mto ule mkubwa, mto wa Frati, nchi yote ya Wahiti, tena mpaka bahari ile kubwa upande wa machweo ya jua, hapo ndipo patakapokuwa mpaka wenu.

 Hapatakuwa mtu ye yote atakayeweza kusimama mbele yako siku zote za maisha yako; kama nilivyokuwa pamoja na Musa, ndivyo nitakavyokuwa pamoja na wewe; sitakupungukia wala sitakuacha. 

Uwe hodari na moyo wa ushujaa, maana ni wewe utakayewarithisha watu hawa nchi hii niliyowaapia baba zao ya kwamba nitawapa.
YOSHUA. 1:3‭-‬6 

Kwa wale waliozaliwa katika agano, uzao uteule watu wa milki ya Mungu  watu walio okoka . Wanao mwamini Yesu kuwa Bwana na mokozi wa maisha yao. 

Watu wenye kuishindania imani...  Mungu amewapa kutawala kila eneo la ardhi wanapo kanyaga. Ila kama unajua kuomba jinsi ya kujiunganisha na ardhi.. na kuomba toba juu ya ardhi ili uweze kupata baraka zilizo kwenye ardhi hiyo.

Haijalishi ardhi hiyo iko katika hali gani. Unachotakiwa kujua kuwa wewe ni mtumishi wa Mungu na unayo mamlaka ya kiagano na muumba wa Mbigu na nchi.. 

Na hii inatukumbusha kuwa kuombea ardhi ya mkoa unao ishi.... au ardhi unayokaa ili baraka zifatane nawe kila uendako. Na kufanya toba ....

Pia tunatakiwa kuwa na moyo wa ushujaa kwa kila kazi iliyo kuwa mbele yetu...  ujasiri ndio utakao tufanya kugundulika kuwa sisi ni wana wa Mungu...  

Tumepewa Moyo wa ushujaa si kwa ajili ya kujihami bali kwa ajili ya watu wanao tuzunguka .. kuanzia ndugu hadi jamii nzima.. kuna wakati wanaitaji msaada wa ki fikra, maombi, uchumi, furaha.. kama tusipokuwa na ujasiri wa kusonga mbele basi kazi iliyotuleta hapa duniani hatujaifanya... 

Mungu ameapa kwamba hatokuacha...zaidi tambua nafasi yako katika jamii...
AMEN

Friday, October 11, 2019

YAKUPASA UFANYE NINI UPATE KUOKOLEWA?


                   
             
          

Bila kuwa na Imani binadamu hatuwezi kupata ukombozi, ukisoma katika waebrania 11:1 inatueleza kuwa basi Imani ni kuwa na uwakika wa mambo yatarajiwayo, ni bayana na mambo yasiyoonekana.

Pia tunasoma katika  (wakorintho 5 :7) biblia iantuambia kuwa maana twaenenda kwa Imani, si kwa kuona,  kwaiyo naweza sema kuwa ukombozi wa mwanadamu unaanzia ndani. Yaani utu wa ndani/ moyoni.  Maana hata Mungu huangalia moyo,

(1samwel 16:7) Lakini Bwana akamwambia Samweli, Usimtazame uso wake, wala urefu wa kimo chake; kwa maana mimi nimemkataa. Bwana haangalii kama binadamu aangaliavyo; maana wanadamu huitazama sura ya nje, bali Bwana huutazama moyo.

 yeye haangalia kama sisi wanadamu kwa macho ya nyama, na hata Mungu akitaka kukujibu maombi yako mchakato wote uanfanywa katika utu wako wa ndani ndipo transformation  inafanyika kuja kwa jinsi ya mwili. Mwanadamu ukiwa vizuri kwenye mambo ya rohoni automatical unakuwa connected na Mungu kwa sababu network ya mawasiliano yenu yanakuwa mazuri,


Kwa maana (warumi 10:9-12) inaeleza kuwa kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa mungu alimfufua katika wafu, utaokoka. Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.


Kwaiyo tunaona kuwa kuamini kunaanzia moyoni lakini pia unatakiwa kile unacho amini ukitamke kwa sauti yaani kwa kinywa ili kiumbike kwa jinsi ya mwili.

25 Lakini panapo usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za kumsifu, na wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza.
26 Ghafula pakawa tetemeko kuu la nchi, hata misingi ya gereza ikatikisika, na mara hiyo milango ikafunguka, vifungo vya wote vikalegezwa.
27 Yule mlinzi wa gereza akaamka, naye alipoona ya kuwa milango ya gereza imefunguka, alifuta upanga, akataka kujiua, akidhani ya kuwa wafungwa wamekimbia.
28 Ila Paulo akapaza sauti yake kwa nguvu, akisema, Usijidhuru, kwa maana sisi sote tupo hapa.
29 Akataka taa ziletwe, akarukia ndani, akitetemeka kwa hofu, akawaangukia Paulo na Sila;
30 kisha akawaleta nje akasema, Bwana zangu, yanipasa nifanye nini nipate kuokoka?
31 Wakamwambia, Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka pamoja na nyumba yako.


Katika vifungu hivyo inaongelea kuhusu Paulo na sila, walipotupwa gerezani, story inatueleza kuwa katika usiku huo walikuwa wakiomba na kumwimbia Mungu nyimbo za kumsifu, yaani walikuwa wana mtukuza  Mungu ghafla pakawa na tetemeko kuu la nchi hata misingi ya gereza ikatikisika, tunaona mlinzi wa gereza alishangaa yaliyotokea akaogopa akataka kujiuwa. Alishangaa na kuogopa aliyo yaona akauliza Bwana zangu, yanipasa nifanye nini nipate kuokoka?paulo na sila wakamjibu MWAMINI BWANA YESU  , mpendwa tunacho takiwa ni kumwani Bwana Yesu kwa kila kazi alizofanya na kuamini kupitia yeye dunia iliokolewa, maana yeye alikufa msalabani kwa ajili yangu mimi na wewe ili tuweze kuishi Maisha ya ushindi hapa duniani.

Yamkini unapita Maisha magumu, nikutie moyo tu ukimwamini Yesu naye hatokuacha uangamie, tena yuko mlangoni mwa moyo wako anabisha hodi, anasema katika....


ufunuo 3:20 Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami. 

 Yesu anatuambia kuwa tukisikia sauti yake na kufungua mioyo yetu aingie ndani yetu, tutakula pamoja nae, hapa anamaana kwamba tutaweza kuzungumza nae na kupeana habari za furaha, anaposema atakula na sisi anamaana hawezi ondoka upesi, ataumega mkate kama kwa wale wanafunzi wa Emmausi ( luka 24:13-35), atakaa na sisi na kutujulisha jinsi ya kupata itaji letu kama alivyowaambia wakina petro pale walipokosa samaki usiku kucha (9 YOHANA 20:1-13), atatupa baraka na kuondoa mapungufu yetu, shida zetu, magojwa yetu.

  Yamkini unasumbuliwa na ulevi mwamini Yesu una umruhusu utapona, yamkini uanteswa na madawa ya kulevya  mwamini yesu utapona. Hakuna mtu alienda kwakwe akatoka bure. Yote kwakwe yanawezekana.  Katika hali hiyohiyo mwamini yesu naye atakusaidia .

Paulo na sila walimwamini mungu katika shida yao, walifungwa mikatare, ndani ya gereza lakini walimuamini yesu, sijui gereza lako ni lipi lakini nina neno moja kwako mwamini YESU, sijui una mikatare gani Maisha mwako yupo Yesu mnazarayo atakufungua ukimwamini…

Hawa watumishi walimtukuza Mungu wakati wa shida, wakati wanauguza majeraha ya mapigo, wanatufundisha kuwa haijalishi unapita katika hali gani ya Maisha, haijalishi unapita katika nyakati gani za Maisha , hajialishi unapita katika majaribu ya namna gani, tunatakiwa tumtukuze Mungu alie hai, kwa maana katika sifa Mungu anashuka, katika Maombi Mungu husikia kilio chetu.

Labda unaweza kusema Maisha yako unapitia katika giza nene ambalo uwezi kuona Maisha yako ya mbele, nikuambie tu mpendwa kuwa usiache kuomba , usiache kumsifu Mungu maana hata wakina Paulo na sila walikuwa katika giza hilo, hawakujua hatima yao ya Maisha ya kesho, walichokuwa wanajua kuwa Yesu ni Bwana.

Yamkini ndugu na marafiki zako  uliokuwa nao katika dhiki hiyo wamekata tamaa wanakushangaa na kusema na kutazama jinsi unavyo mtukuza Mungu na kuomba , usiwasikilize ,usiwatazame, wewe mtukuze Mungu kwa maana hata wakina Paulo na sila wenzao gerezani waliwashangaa hivyo hivyo. Mpaka Bwana aliposhuka kuwakomboa.

UNATAKA KUMPOKEA YESU AWE BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YAKO ?  NA JE LABDA ULIANGUKA KATIKA DHAMBI UNATAKA KUTENGENEZA NA YESU, FUATISHA SALA HII

BWANA YESU NAKUALIKA KATIKA MOYO WANGU, NATUBU DHAMBI ZANGU, NAOMBA UNISAMEHE, NIMEKUKOSEA SANA LAKINI LEO NAFUNGUA MOYO WANGU PIA NASEMA NDIYO KWAKO, NAKUALIKA UWE BWANA WANGU NA MWOKOZI WANGU KWA KUWA WEWE ULIFUFUKA NA MIMI UMENIFUFUA, KWA JINA LAKO YESU KRISTO AMEN…

                                 FURAHIA MAISHA YA USHINDI…..

Makala nyingine

IMPORTANCE OF OUR TESTIMONIES IN THE CHURCH

Mathayo 8:1-4 Naye aliposhuka mlimani, makutano mengi walimfuata.  Na tazama, akaja mtu mwenye ukoma akamsujudia, akisema, Bwana, u...